CAG abaini madudu CWT

Muktasari:

Hayo yamebainishwa katika ripoti ya CAG


Dar es Salaam. Ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) mwaka 2016/17 imebaini madudu katika ukaguzi wa Chama cha Walimu Tanzania (CWT).

Akiwasilisha ripoti  yake ya ukaguzi ya mwaka 2016/17 leo Jumanne Machi 27, 2018 Ikulu Dar es Salaam  ya ukaguzi walioufanya CWT, alisema  wamebaini kuna mambo yanayofanywa kinyume cha matakwa ya kanuni za fedha.

“Kwa mfano kulikuwa na malipo yaliyofikia Sh3.5 bilioni ambazo zilifanywa bila kuidhinishwa na Katibu Mkuu na mweka hazina wa CWT kati ya kipindi cha 2011 na 2016,” amesema CAG, Profesa Mussa Assad .

Amesema ukaguzi wa CWT ulifanyika kwa maombi maalumu kwa kuwa siyo sehemu ya mashirika ya umma na baada ya ukaguzi huo ilibaini taasisi hiyo kutoendeshwa sawa sawa.

 CAG katika mwaka wa fedha unaoishia  Juni, 30 2016 ilibaini kasoro na upungufu katika ukaguzi wa Serikali Kuu, Serikali za mitaa na mashirika ya umma.