Lukuvi awatangazia vita wadaiwa sugu kodi ya ardhi

Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi akizungumza na wadau wa umiliki wa ardhi nchini kutoka kwenye taasisi, mashirika na makampuni yanayodaiwa kodi ya pango la ardhi,  kwenye Ukumbi wa Hazina jijini Dodoma leo. Picha na Edwin Mjwahuzi

Muktasari:

Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi amekutana na wakuu wa taasisi, mashirika na kampuni yanayodaiwa kodi ya pango la ardhi na kutoa siku tisa kwa wadaiwa sugu kulipa kodi hiyo, watakaoshindwa watafikishwa mahakamani


Dodoma. Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi nchini Tanzania, William Lukuvi amesema wadaiwa sugu wa kodi ya ardhi  wataanza kufikishwa mahakamani Juni 21, 2019.

Akizungumza leo Jumanne Juni 11,  2019  Lukuvi amesema kuna taasisi, kampuni na mashirika 207 yanadaiwa zaidi ya Sh200 bilioni.

“Wanatakiwa kulipa kabla ya Juni 20, 2019  ili kukwepa aibu na fedheha,”amesema Lukuvi.

Amesema kuanzia Juni 21, 2019 wasiolipa watafikishwa mahakamani kupitia madalali waliowateua kukamata, kuuza mali zao.

Lukuvi amesema wawakilishi kutoka taasisi 197 kati ya 207 aliowaita katika mkutano huo uliofanyika jijini Dodoma wamehudhuria.

Awali Katibu Mkuu wa Wizara ya Ardhi, Nyumba na Makazi, Dorith  Mwanyika amesema baada ya kuziita  taasisi za Serikali walibaini ambazo hazijalipa kodi tangu mwaka 2012 hadi sasa