Rais Magufuli atoa ndege kusafirisha mwili wa Ruge

Muktasari:

Msemaji wa familia ya Mutahaba amesema Rais Magufuli ametoa ndege hiyo kwa ajili ya kusafirisha mwili wa Ruge kutoka Dar es Salaam kwenda Bukoba


Dar es Salaam. Rais John Magufuli ametoa ndege ya Serikali kwa ajili ya kuusafirisha mwili wa marehemu Ruge Mutahaba utakaopelekwa Bukoba kwa ajili ya kuzika.

Msemaji wa Familia ya Mutahaba, Raymond Kashasha amesema hayo leo Ijumaa,Machi 1 alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari.

Ruge anatarajiwa kuzikwa kijijini kwao Kiziru wilayani Bukoba mkoani Kagera na atasafirishwa kutokea Dar es Salaam siku ya Jumapili, Machi 3.

Pia ametoa ndege ya Air Tanzania kwa ajili ya watu wanaotaka kwenda kumzika Ruge ambayo itaondoka Dar es Salaam siku ya Jumatatu, Machi 4 asubuhi kwa gharama ya Sh 600,000 kwenda na kurudi.

Siku ya Jumatatu ndiyo atakayozikwa Ruge kijijini kwao