VIDEO-Nassari aweka hadharani jinsi madiwani walivyorubuniwa Arusha

Muktasari:

  • -Ushahidi huo ni wa madiwani waliojiuzulu na kuhama Chadema

 Mbunge wa Arumeru Mashariki (Chadema), Joshua Nassari ameweka hadharani ushahidi wa rushwa na waliopewa madiwani ambao wamejiuzulu Chadema.          

Akizungumza na waandishi wa habari leo Jumapili, Nassari ambaye ameambatana na Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless  Lema walitoa  ushahidi huo na kueleza wataukabidhi Takukuru na katika taasisi nyingine.

Katika ushahidi huo viongozi kadhaa wamerekodiwa wakiwashawishi madiwani kuhama na baadhi waliahidiwa wangelipwa posho za vikao vyao vilivyobaki hadi 2020 na kukamilishwa  miradi  yao.

Miongoni mwa makubaliano hayo ni kuwa wapewe fedha na kupata ajira na kukamilishwa miradi yote ya maendeleo waliyoahidi.

Wakati Nassari akifanya hivyo tayari baadhi ya madiwani waliojiuzulu walisema kuwa hawakushawishiwa na mtu yeyote wala kupewa rushwa bali wamehama kuunga mkono juhudi za Rais John Magufuli.