Ahukumiwa miaka 30 jela kwa kumbaka mwanafunzi
Muktasari:
- Wambura Sukuru mkazi wa Mugumu leo Jumanne Oktoba 5, 2021 amehukumiwa kifungo cha miaka 30 jela na kulipa faini ya Sh1 milioni na mahakama ya hakimu mkazi wilaya ya Serengeti kwa kosa la kumbaka mtoto wa miaka 13 na kumpa mimba.
Wambura Sukuru mkazi wa Mugumu leo Jumanne Oktoba 5, 2021 amehukumiwa kifungo cha miaka 30 jela na kulipa faini ya Sh1 milioni na mahakama ya hakimu mkazi wilaya ya Serengeti kwa kosa la kumbaka mtoto wa miaka 13 na kumpa mimba.
Hata hivyo mwanafunzi huyo alifariki dunia baada ya kujifungua kwa njia ya upasuaji.
Hukumu katika kesi ya jinai namba 319/2020 imesomwa na Hakimu Mkazi, Adelina Mzalifu baada ya kuridhika na ushahidi uliotolewa na mashahidi watano upande wa jamhuri.