Balozi Kijazi afariki dunia

Dar es Salaam. Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi amefariki dunia.

Taarifa iliyotolewa na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu,  Gerson Msigwa inasema Balozi Kijazi amefariki dunia leo Jumatano Februari 17, 2021 saa 3 usiku katika Hospitali ya Benjamin Mkapa jijini Dodoma alikokuwa akipatiwa matibabu.

"Taarifa ya mazishi ya Balozi Kijazi itatolewa baadaye, " inaeleza taarifa hiyo.

Endelea kufuatilia Mwananchi