Basi lapata ajali Songwe

New Content Item (1)
New Content Item (1)

Muktasari:

Basi la kampuni ya Kilimanjaro linalofanya safari kutoka Tunduma kwenda Dar es Salaam limepata ajali maeneo ya Senjele mkoani Songwe.

Songwe. Basi la kampuni ya Kilimanjaro linalofanya safari kutoka Tunduma kwenda Dar es Salaam limepata ajali maeneo ya Senjele mkoani Songwe.

Basi hilo limepata ajali leo Jumatatu Machi 14, 2022 asubuhi wakati likielekea Dar es Salaam.

Akizungumza kwa njia ya simu na Mwananchi, Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Songwe, Rashid Ausi amethibitisha kutokea ajali hiyo akisema anaelekea kwenye eneo la tukio.

Bado hakuna taarifa za vifo wala majeruhi zilizoripotiwa mpaka sasa.

Kamanda Ausi ameahidi kutoa taarifa baadaye

Endelea kufuatilia Mwananchi kwa habari zaidi