Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

CCM Arusha yamkaribisha Lowassa nyumbani

Muktasari:

CCM Arusha yamkaribisha nyumbani Lowassa yadai alikuwa safarini sasa amerudi


Arusha. Chama cha Mapinduzi (CCM) mkoa wa Arusha kimemkaribisha nyumbani Waziri Mkuu wa zamani Edward Lowassa na kusema alikuwa safarini amerudi nyumbani.

Akizungumza na Mwananchi leo Ijumaa Machi 1, 2019 Katibu Mwenezi wa CCM mkoa Arusha, Shaban Mdoe amesema Lowassa amefanya uamuzi wa busara kurudi nyumbani.

"Alikuwa safarini amerudi nyumbani, Arusha tutampokea na tunaimani tutashirikiana nae kuhakikisha CCM inashida kwa asilimia 100 uchaguzi serikali za mitaa na pia mwaka 2020 " alisema

Lowassa alijiunga na Chadema mwaka 2015 na kugombea nafasi ya Urais ambapo mkoa wa Arusha ndio uliathirika zaidi na kuhama kwake CCM.

Miongoni mwa viongozi wa CCM waliohama na Lowassa alikuwa Mwenyekiti wa CCM mkoa Arusha, Onesmo Ole Nangole, Katibu Mwenezi Mkoa, Isack Joseph,Mwenyekiti wa UVCCM mkoa Arusha, waliokuwa madiwani zaidi ya 30 na viongozi wengine kadhaa.