Chadema yazungumzia Lowassa kwenda CCM
Muktasari:
Chama kikuu cha upinzani nchini Tanzania cha Chadema kimesema hatiwezi kutikisika wala kuyumba kutokana na uamuzi uliochukuliwa na mwanachama wa chama hicho, Edward Lowassa
Dar es Salaam. Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) nchini Tanzania kimesema kuondoka kwa mwanachama wake, Edward Lowassa na kurejea Chama cha Mapinduzi (CCM) hakutakuwa na madhara yoyote.
Hayo yamesemwa leo Ijumaa Machi 1, 2019 na Katibu Mkuu wa chama hicho kikuu cha upinzani Tanzania, Dk Vicent Mashinji alipozungumza na Mwananchi muda mfupi baada ya Lowassa ambaye ni waziri mkuu wa zamani kutangaza uamuzi huo.
“Tunamtakia maisha mema huko aendapo yeye ni mtu mzima anajua anachokifanya,” amesema Dk Mashinji.
Alipoulizwa iwapo uamuzi wa Lowassa unaweza kukitetelesha chama hicho kikuu cha upinzani Dk Mashinji amejibu kwa kifupi “It will never happen (haiwezi kutokea)”.
Endelea kufuatilia Mwananchi kwa taarifa zaidi