DPP asamehe wafungwa 183 Karagwe

DPP asamehe wafungwa 183 Karagwe

Muktasari:

Mkurugenzi wa Mashtaka nchini (DDP), Biswalo Mganga amewafutia mashtaka mahabusu 183 katika magereza ya Karagwe, Bukoba, Biharamulo na Muleba mkoani Kagera.

Karagwe. Mkurugenzi wa Mashtaka nchini (DDP), Biswalo Mganga amewafutia mashtaka mahabusu 183 katika magereza ya Karagwe, Bukoba, Biharamulo na Muleba mkoani Kagera.

Amesema hayo leo  Alhamisi Januari 21, 2021 katika ziara yake ya kikazi Wilaya ya Karagwe  mkoani Kagera.

Amesema baada ya kutembelea katika magereza hizo na kuzungumza  na mahabusu amewafutia mashtaka  mahabusu 57 wa Wilaya ya Karagwe, Bukoba 54, Biharamulo 48 na Muleba  26.

Amewataka wananchi kuishi nao vizuri wanaporejea uraiani ili kujenga jamii yenye amani, upendo na mshikamano.

Mganga amesema kuwa katika ziara yake hiyo ya kutembelea magereza alikuta wahamiaji haramu 15 waliokaribishw ana wananchi ambao ni wenyeji wa mkoa huu. 

Jaji wa mahakama kuu Kanda ya Kagera, Ntemi Kilekamajenga

amesema Mkoa wa Kagera unaongoza kwa kuwa na kesi nyingi za mauaji na kuwaomba viongozi  wa dini kuhubiri amani.

Amesema kesi nyingi zingeweza kumalizwa kwa njia ya usuluhishi nje ya mahakama hivyo kuipunguzia Serikali gharama za uendeshaji  wa kesi.

Jaji Kilekamajenga amesema katika mkoa wa Kagera kesi ambazo zipo katika hatua ya kusikilizwa zinakaribia kuvuka 450 hivyo mkoa wa Kagera  unaweza kuwa wa pili au watatu kwa Tanzania kuwa na kesi nyingi za mauaji.

Katika hatua nyingine amezindua ofisi ya mwendesha mashtaka Wilaya ya Karagwe  ili kuwapunguzia gharama wananchi na kupunguza ucheleweshaji wa mashauri mahakaman