Kanisa lawaita wananchi wakahamishe makaburi ya wapendwa wao
Muktasari:
- Wakazi wa Vwawa wilayani Mbozi Mkoa wa Songwe waliozika ndugu katika makaburi ya Kanisa Katoliki la Mtakatifu Patrick Parokia ya Vwawa wametakiwa kufika kanisani hapo kupata utaratibu wa kuhamisha makaburi.
Songwe. Wakazi wa Vwawa wilayani Mbozi Mkoa wa Songwe waliozika ndugu katika makaburi ya Kanisa Katoliki la Mtakatifu Patrick Parokia ya Vwawa wametakiwa kufika kanisani hapo kupata utaratibu wa kuhamisha makaburi.
Paroko wa Parokia hiyo, Padri Dennis Hula amesema hayo alipozungumza na Mwananchi Digital jana Desemba17, 2021 ofisini kwake kuwa wamepanga kuhamisha makaburi hayo kwa kuwa wanahitaji eneo hilo kwa matumizi mengine na ni eneo la kanisa hilo.
"Tunaheshimu marehemu na tunajali utu kwa hiyo ndio sababu tumeamua kutangaza kwamba kila ambaye anajua ameshawahi kuzika ndugu yake katika eneo hili aje atoe taarifa zilizokamili na ikipendeza aje na watu kadhaa waliyoshuhudia Ili taratibu ziweze kuchukuliwa na kanisa," amesema.
Mkazi wa Vwawa, Yusta Kayuni amesema itakuwa mara ya kwanza kwake tangu azaliwe kuona makaburi yanahamishwa licha ya kuwa ana ndugu zake watatu waliozikwa hapo.
"Najiuliza sana siku itakapofika siku ya kuyaondoa masalia ya ndugu zangu itakuwaje sipati majibu," amesema