Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Mbaroni akidaiwa kufukua kaburi

Muktasari:

Kamanda wa Polisi mkoani hapa, Dhahiri Kidavashari amesema jana kuwa  mtuhumiwa huyo (jina linahifadhiwa) alikamatwa usiku wa kuamkia jana akiwa na majembe na koleo.

Mbeya. Mkazi wa Kijiji cha Chapakazi, Mbeya Vijijini amekamatwa na polisi kwa kwa tuhuma za kufukua kaburi alilozikwa mtu aliyekuwa na ulemavu wa ngozi, (albino), mwaka 2010.

Kamanda wa Polisi mkoani hapa, Dhahiri Kidavashari amesema jana kuwa  mtuhumiwa huyo (jina linahifadhiwa) alikamatwa usiku wa kuamkia jana akiwa na majembe na koleo.

Kidavashari amesema kaburi alilokuwa akifukua alizikwa Sister Osisara ambaye alikuwa albino.

Amesema marehemu alifariki dunia mwaka 2010 kwa ugonjwa wa homa na kuzikwa katika makaburi ya Kijiji cha Mumba ambako mtuhumiwa alikutwa akifukua kaburi lake.