Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Mgambo wavunja meza za wauza magazeti Dodoma

Muktasari:

Mgambo wa Jiji la Dodoma wamevunja meza za wauza  magazeti na kuchukua magazeti yaliyokuwa yakiuzwa hivyo kusababisha taharuki kwa wafanyabiashara hao.


Dodoma. Mgambo wa Jiji la Dodoma wamevunja meza za wauza  magazeti na kuchukua magazeti yaliyokuwa yakiuzwa hivyo kusababisha taharuki kwa wafanyabiashara hao.

Kuvunjwa kwa meza hizo kunatokana na operesheni ya Jiji la Dodoma ya kuwaondoa wamachinga wote waliopo katikati ya Jiji  iliyoanza Oktoba 31 mwaka huu.

Wamachinga hao wamemishiwa katika soko la Machinga lililopo Bahiroad Jijini hapa.

Hata hivyo wauza magazeti hao walikuwa wakiendelea na biashara kama kawaida kabla ya jana kutoka agizo kwa Mkurugenzi wa Jiji Joseph Mafuru kwamba wanatakiwa kuondoa meza zao.

Mwananchi imeshuhudia  leo Novemba 19 ,2022  saa nne asubuhi  askari hao na baadhi ya watumishi wa Jiji hilo wakiwa katika gari lenye namba za usajili DFPA 6898 Nissan Double Cabin katika mtaa wa Independence Kata ya Majengo wakivunja meza ya muuza magazeti na  kisha kuchukua magazeti kwa nguvu.

Mara baada ya kuivunja meza hiyo waliipakia katika gari pamoja na magazeti na kisha kuondoka nayo.

Muuzaji wa meza hiyo, Mwajuma Kisungura amesema anashangaa kuona mgambo hao wakimvunjia pamoja na kumchukulia magazeti yake.

“Nitarejesha nini jioni magazeti yangu yote wameyachukua kwanini wanatuonea hivi tumewakosea nini? Alihoji muuzaji huyo.

Rehema Ahmed amesema Jiji linajichanganya kwani wauza magazeti wanatakiwa kuwepo katikati ya Jiji.

Akilitolea ufafanuzi hilo,Mkurugenzi  Mafuru amesema katika kuwahamisha wamachinga wamekutana na changamoto ya kutokuwepo kwa maeneo ya wauza magazeti, shoe shine na bodaboda.

Amesema  wanaandaa maeneo yao katika soko la wamachinga na mpaka Jumatatu utaratibu utakuwa upo vizuri. 

“Wakati wa zoezi hili tuliwaondoa wote kabisa lakini tutawarudisha kwa kuwapanga wiki ijayo kuanzia Jumatatu wasiwe na wasiwasi tutakuwa tumeishakamilisha vichanja vyao,”amesema  Mkurugenzi Mafuru.