Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Naibu Waziri kuongoza hafla ya kuaga miili ya wanafamilia watatu

Muktasari:

  • Naibu Waziri, Ofisi ya Rais Utumishi na Utawala Bora, Deogratius Ndejembi, kuongoza hafla ya kuaga mili ya wanafamilia watatu waliopoteza maisha Kwa ajali ya gari Agosti 2 Mwaka huu Bagamoyo.

Dar es Salaam. Naibu Waziri, Ofisi ya Rais Utumishi na Utawala Bora, Deogratius Ndejembi na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila wanaotarajiwa kuongoza waombolezaji, kuaga miili ya wanafamilia watatu kati ya wanne waliofaliki katika ajali ya gari.

 Kwa mujibu wa mshehereshaji (MC) wa shughuli hiyo, Aminata Juma, kutoka Shirika la Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF), kiongozi mwingine ni Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Jumanne Muliro.

Shughuli hiyo inahusisha kuaga miili ya wanafamilia ahao ambao ni Sia Msuya, Dk Norah Msuya na Diana Msuya, waliopoteza maisha katika ajali iliyotokea wilayani Chalinze usiku wa Agosti 2, Mwaka huu wakiwa safarini kuelekea msibani wilayani Same.

"Naibu Waziri, Ofisi ya Rais Utumishi na Utawala Bora, Deogratius Ndejembi, Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila na Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Jumanne Muliro ni baadhi ya viongozi wa kiserikali tunaotegemea kuwapokea," amesema Aminata

Neech ambaye ndiye alikua kaka pekee katika familia hiyo, na ndiye aliyekuwa dereva wa gari hiyo, alizikwa Agosti 6 kijijini kwao Msangeni Ugweno Wilaya ya Mwanga, mkoani Kilimanjaro.

Na leo Agosti 8 ndiyo siku ambayo ndugu waliosalia watazikwa katika makaburi ya Ununio kwa Kondo baada ya kuagwa katika viwanja vya gofu Kawe jijini Dar es Salaam.