Rayvanny wa WCB kuwasili nchini leo

Muktasari:

  • Rayvanny alipata tuzo hiyo nchini Marekani Juni 25 na kuwa msanii wa kwanza kushinda tuzo hizo kubwa.

 Msanii wa kizazi kipya, Rayvanny aliyeshinda tuzo ya BET kipengele cha International Viewers Act 2017, atawasili nchini leo saa 8 mchana katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA)

Rayvanny alipata tuzo hiyo nchini Marekani Juni 25 na kuwa msanii wa kwanza kushinda tuzo hizo kubwa.

Rayvanny ameambatana na Babutale ambaye ni mmoja wa mameneja wa Kundi la WCB.

Meneja wake, Makame Fumbwe amesema, Rayvanny atakapowasili, msafara wake utatoka JNIA na kupita katika mitaa mbalimbali ya jiji na baadaye atakwenda katika mahojiano kwenye kituo cha Clouds.