Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

RC Kagaigai awataka viongozi wa dini kuliombea Taifa

New Content Item (1)
RC Kagaigai awataka viongozi wa dini kuliombea Taifa

Muktasari:

  • Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Dk Stephen Kagaigai amewataka waumini na viongozi wa dini kuendelea  kuliombea Taifa hasa katika kipindi hiki cha  maambukizi ya ugonjwa wa Covid-19.

Moshi. Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Dk Stephen Kagaigai amewataka waumini na viongozi wa dini kuendelea  kuliombea Taifa hasa katika kipindi hiki cha  maambukizi ya ugonjwa wa Covid-19.

Amewataka viongozi wa dini kuendelea kuwasisitiza waumini kuchukua tahadhari za ugonjwa huo na kuhakikisha miongozo  inayotolewa na Wizara ya Afya inazingatiwa.

Ameeleza hayo leo Jumamosi Juni 27,  2021  katika Kanisa la Kilimanajro Revival Temple (TAG) lilipo Moshi  Mjini.

"Tuendelee kushirikiana kuliombea  Taifa letu hasa katika kipindi hiki ambacho  dunia inapita katika janga hili la corona, tuendelee kuzingatia miongozo inayotolewa na Wizara ya Afya ili tuvuke wote salama."

"Kuvaa barakoa ni muhimu  hasa mnapokuwa kwenye msongamano, hakikisheni mnanawa mikono kwa sabuni kwa kutumia maji tiririka na sehemu ambayo hakuna maji tumieni vitakasa mikono," amesema Kagaigai.



Mbali na corona amewataka viongozi wa dini mkoani humo kushirikiana naye kukemea maovu ikiwemo unywaji wa pombe uliopindukia  ambao unarudisha nyuma maendeleo ya Taifa na kwa mtu mmoja mmoja.



"Wachungaji pamoja na waumini mliopo hapa, tushirikiane pamoja na kukemea  yanayoturudisha nyuma kimaendeleo, kuna vijana sasa hivi wamejiingiza kwenye ulevi,  ni jukumu letu sote kushirikiana  kukemea haya yote," amesema Kagaigai


Mchungaji wa kanisa hilo, Ron Swai amesema wataendelea kushirikiana na mkuu huyo wa mkoa kuhakikisha  yote yanayotakiwa kufanyika yanatimizwa.