Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Tembo wazua kizaazaa vijiji saba Nachingwea

Tembo wazua kizaazaa vijiji saba Nachingwea

Muktasari:

  • Wakazi wa vijiji saba wilayani Nachingwea wanaishi  kwa hofu baada ya tembo kuvamia  vijiji hivyo na kuharibu  mazao na kujeruhi mtu mmoja.

Nachingwea. Wakazi wa vijiji saba wilayani Nachingwea wanaishi  kwa hofu baada ya tembo kuvamia  vijiji hivyo na kuharibu  mazao na kujeruhi mtu mmoja.

Mkuu wa Wilaya ya Nachingwea,   Hashimu Komba amesema tembo hao wamesababisha madhara makubwa na zimefanyika jitihada mbalimbali  kuwaondoa kwa mara ya kwanza lakini wamerudi.

“Ni kweli huwa tunapata changamoto ya tembo kurudi kwenye makazi ya watu mara kwa mara hata hivyo tulishawahi kupokea taarifa ya kuonekana kwa wanyamapori  hao katika vijiji mbalimbali kikiwemo cha Ilolo, Nyambi B, Ndangambo, Mbute, Nanjili  na Namatekwe."

“Maofisa wetu wa idara ya wanyamapori walichukua hatua na kuanza kuwahamisha wanyama hao kutoka kwenye makazi ya watu lakini tuliongezewa nguvu kutoka Seluu walituletea askari watano.”

Katika ufafanuzi wake amesema,  “unajua tembo wanapoondoka huwa wana desturi ya kurudi,  sasa wamerudi  mara ya pili wamesababisha madhara kwenye mazao na kujeruhi mtu mmoja ambaye anadaiwa kufariki.”

“Unajua uwepo wa wanyama hao ni matokeo ya uhifadhi mzuri wa mazingira na udhibiti wa majangili hii ndio inapelekea kutawanyika katika maeneo mengi."