Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Upelelezi kesi dhidi ya Halima Mdee wakamilika

Muktasari:

  • Upande wa mashtaka umesema umekamilisha upelelezi wa shauri dhidi ya Halima Mdee.

Dar es salaam. Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, imepanga Oktoba 11 kumsomea maelezo ya awali Mbunge wa Kawe (Chedema), Halima Mdee.

Mbunge huyo anakabiliwa na kesi ya kutoa lugha ya matusi dhidi ya Rais John Magufuli.

Wakili wa Serikali Mwandamizi, Mutalemwa Kishenyi mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Victoria Nongwa amesema upelelezi wa kesi umekamilika, hivyo kuomba shauri hilo lipangiwe tarehe kwa ajili ya kumsomewa mshtakiwa maelezo ya awali.

Hakimu Nongwa ameahirisha kesi hiyo hadi Oktoba 11.

Mdee anakabiliwa na shtaka la moja la kutumia lugha ya matusi dhidi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Mdee anadaiwa kutenda kosa hilo Julai 4 makao makuu ya Chadema Kinondoni jijini Dar es Salaam.

Anadaiwa kutamka kuwa Rais anazungumza  ovyo ovyo na anatakiwa afungwe break, kauli inayodaiwa ingeweza kusababisha uvunjifu wa amani.