Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

VIDEO: Meya ataja sababu kuwataka wajumbe kikaoni kuvua barakoa

Meya ataja sababu kuwataka wajumbe kikaoni kuvua barakoa

Muktasari:

  • Meya wa manispaa ya Moshi, Juma Raibu amesema aliwataka  wajumbe waliokuwa wamevaa barakoa katika kikao cha bajeti cha baraza la madiwani  manispaa hiyo kuzivua kwa sababu  uvaaji huo huongea hofu ya ugonjwa wa corona kwa wananchi.

Moshi. Meya wa manispaa ya Moshi, Juma Raibu amesema aliwataka  wajumbe waliokuwa wamevaa barakoa katika kikao cha bajeti cha baraza la madiwani  manispaa hiyo kuzivua kwa sababu  uvaaji huo huongeza hofu ya ugonjwa wa corona kwa wananchi.

Ameeleza hayo leo Alhamisi Januari 28, 2021 baada ya kupitisha bajeti ya manispaa hiyo, akibainisha kuwa pamoja na kutakiwa kuchukua tahadhari haitakiwi kupeana hofu

"Nimeona katika baraza madiwani  karibu thelathini, wapo viongozi wa serikali na viongozi wa vyama  walioalikwa  wote hawa  hawajavaa barakoa hata mmoja,  lakini limekuja kundi la watu wamevaa barakoa jambo ambalo wanaamini halmashauri hii ina corona.”

"Nimewaambia wavue waendelee kuamini kuwa corona ipo na tujiendelee kujikinga  lakini manispaa ya Moshi haina corona, tuendelee kujikinga katika mambo mengine ila tusitiane hofu, katika baraza langu la manispaa sitaruhusu mtu yeyote kuingia na barakoa katika kikao changu  kwani ninaamini tuko salama,” amesema.

Akizungumzia hatua ya kuamriwa kuvua barakoa mmoja wa wajumbe katika kikao hicho, Mwanahawa Amir amesema alipokea agizo hilo na kwamba anaamini Tanzania ipo salama kwa kuwa madiwani wote waliokuwa katika kikao hicho walikuwa hawajavaa barakoa.