Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Wafanyabiashara Maswa walilia elimu ya tozo

Baadhi ya wafanyabiashara wilayani Maswa wakiwa katika mafunzo ya mabadiliko ya Sheria ya Kodi ya Mwaka 2022. Picha na Samirah Yusuph

Muktasari:

  • Baadhi ya wafanyabiashara wilayani Maswa Mkoa wa Simiyu waimeiomba Mamlaka ya Mapato (TRA) kutumia lugha za kiungwana zinazoshawiahi wananchi kulipa Kodi.

Maswa. Baadhi ya Wafanyabiashara wilayani Maswa Mkoa wa Simiyu waimeiomba Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kutumia lugha za kiungwana zinazoshawiahi wananchi kulipa Kodi.

Wakiwa katika mafunzo na maofisa wa TRA yenye  lengo la kujenga uelewa wa mabadiliko  ya  kodi  kulingana  na Sheria  ya  Fedha  ya  mwaka 2022 leo Septemba 19, wamesema licha ya kuwa ulipaji wa kodi upo kisheria, maofisa wa mamlaka hiyo wanapaswa kuwa na kauli zenye ushawishi.

“Hakuna haja ya kuwapa wateja vitisho na mlolongo mrefu wa maelezo yanayokatisha tamaa kwa walipa kodi na kusababisha maisha ya kukwepana na kukimbizana.

“TRA ijenge mahusiano mzuri na wafanyabiashara ili kila Mtanzania awiwe na kuona anawajibu wa kutoa kodi ili kuchangia maendeleo," amesema James Nila mfanyabiashara wilayani Maswa.

Kwa upande wake Meneja TRA Mkoa wa Simiyu, Naye Mtandika amesema pamoja na mabadiliko ya sheria, wanajukumu la kuwakumbusha wajibu wa msingi wa kulipa kodi kwa hiari bila kufukuzana wala kukimbizana.

Akizungumza katika mafunzo hayo Mkuu wa Wilaya  ya Maswa, Aswege Kaminyoge amesema kuwa   wananchi  wanatakiwa  kuwa  wazalendo kwa  kulipa kodi ya serikali kwa  maendeleo  ya  Taifa.

“Serikali haifanyi biashara, inakusaya kodi kwa  ajili ya  kazi  za maendeleo, sasa jambo  kubwa  kwa  wananchi  ni  kulipa  kodi  na  serikali inarudisha kodi  hizo kwa ajili ya  maendeleo ya wananchi.

Katika mwaka wa fedha wa 2021/2022 Wilaya ya Maswa ilikusanya Sh717 milioni sawa asilimia 92 ya lengo la ukusanyaji wa mapato ambapo mwaka huu 2012/2023 lengo llililowekwa ni Sh 940.3 milioni.