Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Wateja benki ya FBME walipwa Sh2.42 bilioni

Wateja benki ya FBME walipwa Sh2.42 bilioni

Muktasari:

  • Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Mwanaidi Ali Khamis amesema  Sh2.42 bilioni  zimelipwa  kwa  wateja  wenye  amana katika benki ya FBME sawa na   asilimia   52.13 ya Sh4.65 bilioni  zinazotakiwa kulipwa kwa wateja hao.

Dodoma.  Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Mwanaidi Ali Khamis amesema  Sh2.42 bilioni  zimelipwa  kwa  wateja  wenye  amana katika benki ya FBME sawa na   asilimia   52.13 ya Sh4.65 bilioni  zinazotakiwa kulipwa kwa wateja hao.

Ameeleza hayo leo Jumatano Februari 3, 2021 bungeni mjini Dodoma wakati akijibu swali la mbunge wa Jang'ombe (CCM) Ali Hassan King.

"Serikali  imefikia  hatua  gani  katika  kufuatilia  fedha  za  wananchi  zilizopo katika benki ambazo zimezuiwa kuendesha shughuli zao nchini,” amehoji King.

Akijibu swali hilo, Mwanaidi amesema  mwaka  2017  na  2018  Benki  Kuu  ya  Tanzania (BoT)  ilizifutia leseni  ya  kufanya  biashara  ya  kibenki  benki  saba kwa  mujibu  wa vifungu vya sheria  ya  mabenki  na  taasisi  za  fedha  ya mwaka  2006.

Amezitaja benki  zilizofutiwa  leseni  ya kufanya  biashara  nchini  ni  pamoja  na FBME Bank Ltd,  Mbinga Community Bank Plc, Njombe Community Bank Ltd, Kagera Farmers’ Cooperative Bank Ltd, Meru Community Bank Ltd, Efatha Bank Ltd na Covenant Bank for Women (T) Limited.

Amesema  baada  ya  kuzifutia  leseni  benki  hizo,  BoT iliiteua bodi ya bima ya Amana (Deposit Insurance Board –DIB) kuwa mfilisi.

Amebainisha kuwa katika kutimiza  wajibu  wake  wa  msingi  kisheria,  bodi  ya  bima  ya  Amana  ilianza  shughuli ya kulipa  fidia  ya  bima  ya  amana  ya  hadi  Sh1.5 milioni  kwa  waliostahili  kulipwa  bima katika Benki hizo na shughuli hiyo bado linaendelea kwa wateja ambao hawajajitokeza  kuchukua  fidia.   

Amesema sanjari  na  zoezi  hilo,  DIB  inaendelea  na  kazi ya ufilisi wa benki hizo.

"Hadi kufikia  mwishoni  mwa  mwezi  Desemba 2020 jumla  ya Sh4.94 bilioni  zimeshalipwa  kwa  wateja  wenye  amana  wa  benki  sita  za wananchi (Community Banks) kama zilivyotajwa hapo juu ukiiondoa Benki ya FBME," amesema.

Amesema malipo  hayo  ni  sawa  na  asilimia  77.27  ya  kiasi  cha  Sh6.39 bilioni zilizotengwa kwa ajili ya kulipa fidia.

Mwanaidi amesema wateja waliolipwa ni 21,675 kati ya wateja 57,076 ikiwa ni asilimia 37.98 ya wateja waliokuwa na amana zilizostahili fidia.

Kuhusu Benki ya FBME, Mwanaidi amesema hadi mwishoni mwa  Desemba 2020, Sh2.42 bilioni  zimelipwa  kwa  wateja  wenye  amana ambazo  ni  sawa na   asilimia   52.13   ya   kiasi   cha  Sh4.65 bilioni.

Amesema wateja waliolipwa  ni  3,443  kati  ya  wateja  6,628 ambao ni sawa na asilimia 51.95 ya wateja waliokuwa na amana zilizostahili fidia.

Amesema wateja  waliokuwa  na  amana  inayozidi  Sh1.5 milioni watalipwa kiasi kilichobakia chini ya kazi ya  ufilisi ambapo kwa mujibu wa sheria na taratibu  za  ufilisi  kiasi  kitakacholipwa  kitategemea  fedha  zitakazopatikana  kutokana na  kuuza  mali  za  Benki  husika.

Amesema ukusanyaji  madeni  na  mali  za  benki  hizo linaendelea ili kupata fedha za kuwalipa wateja wenye amana za  zaidi ya Sh1.5 milioni.