Watu watatu wafa kwa kuangukiwa na kifusi Kigogo Fresh
Picha na Jeshi la Polisi
Muktasari:
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ilala, Salum Hamduni amesema leo kuwa ajali hiyo ilitokea saa 8 jana 8:30 mchana na watu wao ni Amos, Rashid na Boniface wanaokadiriwa kuwa na miaka 28-30.
Dar es Salaam. Watu watatu wamefariki na mmoja kujeruhiwa baada ya kuangukiwa na kifusi maeneo ya Kigogo Fresh jijini hapa.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ilala, Salum Hamduni amesema leo kuwa ajali hiyo ilitokea saa 8 jana 8:30 mchana na watu wao ni Amos, Rashid na Boniface wanaokadiriwa kuwa na miaka 28-30.
"Mwili wa Amos umeifadhiwa katika chumba cha kuifadhia maiti Hospitali ya Taifa Muhimbili, wengine wamekwama na tunafanya mpango wa kuleta kifaa kuchimba," amesema Hamduni.
Hamduni amesema majeruhi mmoja amevunjika mguu.