Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Waziri Mkenda amlilia Mramba

Muktasari:

  • Mbunge wa jimbo la Rombo ambaye pia ni Waziri wa kilimo nchini Tanzania, Profesa Adolf Mkenda amesema amepokea kwa masikitiko kifo cha aliyekuwa mbunge wa zamani  wa jimbo hilo, Basil Mramba kilichotokea leo Jumanne Agosti 17, 2021 jijini Dar es Salaam.

Rombo. Mbunge wa jimbo la Rombo ambaye pia ni Waziri wa kilimo nchini Tanzania, Profesa Adolf Mkenda amesema amepokea kwa masikitiko kifo cha aliyekuwa mbunge wa zamani  wa jimbo hilo, Basil Mramba kilichotokea leo Jumanne Agosti 17, 2021 jijini Dar es Salaam.

Akizungumza leo Profesa Mkenda amesema Mramba alitumia nafasi yake ya ubunge kujenga na kuendeleza Wilaya ya Rombo kwa miaka 20 ya ubunge wake na kusema atakumbukwa kwa mengi.

"Sisi wana Rombo tutamkumbuka Mramba kwa mengi na hatutasahau kamwe maendeleo aliyotuletea," amesema Profesa Mkenda

"Historia ya Maisha wasifu na haiba yake vilitosha kumfanya kuwa ni kiongozi wa kutegemewa na sisi sote hata baada ya kuondoka kwenye nafasi rasmi ya uongozi wa kisiasa, tumempoteza kiongozi shupavu ,mwenye busara ,mvumilivu na muungwana,"

 Mkenda amesema Mramba ambaye aliwahi kuwa katika wizara mbalimbali atakumbukwa kwa utumishi wake uliotukuka.

"Kati ya mambo ambayo Mramba atakumbukwa nayo ni juhudi zake za kuimarisha mazingira ya biashara  na uwekezaji hapa nchni, wengi tutamkumbuka jinsi akiwa Waziri wa fedha aliondoa kodi na tozo ambazo zilikuwa kero kwenye uchumi wetu," amesema Waziri Mkenda.