Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Zuma ahukumiwa kifungo cha miezi 15 jela

Zuma ahukumiwa kifungo cha miezi 15 jela

Muktasari:

Mahakama ya Katiba nchini Afrika Kusini imemhukumu kifungo cha miezi 15 jela aliyekuwa rais wa Taifa hilo, Jacob Zuma.

Mahakama ya Katiba nchini Afrika Kusini imemhukumu kifungo cha miezi 15 jela aliyekuwa rais wa Taifa hilo, Jacob Zuma.

Ni baada ya kukutwa na hatia ya  kukaidi agizo la kufika mahakamani baada ya kutoonekana katika kikao cha uchunguzi wa kesi ya ufisadi wakati alipokuwa rais.

Mwenyekiti wa kamati maalum ya uchunguzi wa mahakama, Raymond Zondo ambayo imekuwa ikichunguza madai hayo, aliiomba mahakama itamke kuwa rais huyo wa zamani alidharau mahakama na imhukumu kifungo cha miaka miwili.

Tangu alipojiuzulu mwaka 2018,  Zuma amekuwa akifika mahakamani kujibu mashtaka ya ufisadi ambayo mara kadhaa ameyakanusha.