Sikukuu za wanawake ni kubwa kuliko Krismasi na Eid?

Muktasari:

  • ‘Pisi’ zinaiteka dunia kwa staili wa Nuhu. Yaani siku zao wamezifanya kama vile ‘Lisafina’ kuuubwa linaloelea juu ya uso wa dunia na kukusanya kila kitu. Yaani masela nao wanashadadia sana siku za ‘pisi kali’ kuliko hata singeli michano.

Kama bado hujagundua hili, basi pole yako. Sikukuu za wanawake ‘nau deizi zimetekova’, zinapewa uzito kuliko sikukuu kongwe kama Krismasi na Eid El Fitr. Achana na Mei Mosi, Sabasaba na kenge kenge zingine. Shitukeni wajomba.

‘Pisi’ zinaiteka dunia kwa staili wa Nuhu. Yaani siku zao wamezifanya kama vile ‘Lisafina’ kuuubwa linaloelea juu ya uso wa dunia na kukusanya kila kitu. Yaani masela nao wanashadadia sana siku za ‘pisi kali’ kuliko hata singeli michano.

Nenda kwenye vyama vya siasa huko, jumuiya za kina mama zina nguvu sana. Mitaani shughuli zao zinavuruga. Na bahati mbaya washua ‘wanadedi’ sana. Kiasi kwamba watoto wa kiume wanakosa watu wa kuwatazama kama vioo vyao. Wanaishi bila kioo.

Yaani mtoto wa kiume anazaliwa na ‘singo mama’. Anakutana na mama na bibi yake. Babu alishadedi na baba yake aliingia mitini kukwepa malezi. Yaani dogo anaona mitikasi ya kike tu toka anapozaliwa hadi anabalehe. Hata wa kiume waliopo wana swaga za mama yake.

Kaka zao wa mitaani wanadekadeka kama dada zao. Watoto wengi kwa sasa hawana ukamilifu wa kiumeni. Sababu kubwa ni kutwa kuzungukwa na pigo na staili za kikeni zaidi. Kuanzia nyumbani, mitaani na hata shuleni. Inakata stimu sana basi tu.

Unachotakiwa kujua ni kwamba hii dunia ina wa kike wengi kuliko wa kiume. Na wa kiume wachache waliopo katikati yao wengi wana pigo za kidada. Kwa sababu ya aina ya malezi wanayopata kwa sasa. Watoto wetu wanalelewa sana kikeni kwa changamoto nyingi sana.
Usishangae mshikaji wako kinomanoma wa kiume. Usiku anampigia simu ‘demu’ flani ili wakutete wewe. Yaani anaweka vocha anampigia demu wa mtaani au ofisini kwenu. 

Wanapigania simu kisha wanaanza kushirikiana kukuteta wewe mwanaume mwenzake.
Kwa sababu akili za masela wa dunia ya 2000 za upande wa pili. Tunalelewa kike zaidi vijana wetu. Haina ubaya kulelewa kikeni, ila ubaya unakuja kwenye makuzi yake nje ya jinsi yake. Kitabia, kinaumbile na hata kihisia. Hili zigo ni letu wazee wa kiume.

Wakati tunakua, tuliwakuta baba zetu. Wajomba zetu. Kaka zetu na babu zetu. Wao walikuwa kama taa zetu. Maisha yao yalifanya tujue tofauti ya kikeni na kiumeni. Lakini sasa hivi dada zao wanalelewa kama baba zao. Na kaka zao wanapenda umbea kama mama zao.

Wakati tunakuwa watoto wa kiume tulifanyishwa kazi ngumu ngumu tupu. Tulikomazwa kiakili, kitabia na kimwili. Yaani tungeambiwa hilo gunia bebeni watoto wa kiume. Halafu tungepigwa kama tungekutwa tunacheza mdako au marede au kuvaa kike kike. Noma!
Ndani ya miaka minne tu.

Mimi tayari nilishajua huu ni umama na ubaba kwa namna ya kuishi. Kwa kuwatazama wajomba zangu, kaka zangu na babu zangu. Sisi tulitengenezewa mipira ya kusokotwa (sodo). Watoto wa kike walipewa ukili wasukane.

Sisi tulikalishwa sebuleni, vibarazani au mbele ya nyumba. Tujadili mambo yetu ya soka na mifugo. Kina dada walikaa jikoni au nyuma ya nyumba wapige stori zao za umbea. Yaani hata maeneo ya kukaa na kupiga stori yalitengwa kwa namna ya jinsia zetu.
Lakini hivi sasa watoto wa kiume wapo jikoni kupiga umbea. Watoto wa kiume unawakuta salon za kike wanapiga stori. Hata kwenye hizi kurasa za mitandaoni watoto wa kiume wa mapozi ya dada zao. Siyo kosa lao ni kosa letu wazazi ambao tumeifanya dunia iwe ya kipimbi.

Leo hii unakuta kina dada wamemfunga mtoto wa kiume kanga. Wanacheka akikatika ama akipiga ‘katiwoku’ kama ‘mamisi’ vile. Na kuna kenge zingine zinamrekodi na kurusha mitandaoni. Wanaona ufahari. Mtoto wa kiume mapema tu anaandaliwa kuwa wakike.

Hata kesi za kufumaniwa zimetoweka sana miaka ya karibuni. Kwa sababu vishababi hakuna. Kijana unamuacha na ‘pisi kali’ unaondoka kwa saa kadhaa na ukirudi unawakuta palepale, vilevile na kapozi kalekale. Eti wanaoneshana video za ‘Mondi’ na Zuchu au umbea wa Mange.

Ni wachache ambao utawakuta wanabishana kuhusu goli la Aziz Ki. Wengi wako ‘bize’ na vitu laini kama waini. Dunia ya sasa inamfanya kijana wa kiume awe laini kwa kila kitu. Hata muziki wa sasa mwingi wa kubinuka binuka tu kwa mitindo ya vijana laini laini.

Unabisha? Fuatilia staili ya kucheza ya Amapiano. Ni kujibinua binua tu hata hawaeleweki. Watoto ‘wanalefti grupu’ kibwegebwege. Kuna ‘taimu’ natamani niwe Rais niamrishe nchi nzima namna ya watoto wa kiume hawa kuishi kiume kama kiume. Tumechoka kuwapoteza kinyendo.

Mara ya mwisho kuwakuta watoto wanatwangana ngumi mtaani kwako ni lini? Zamani kila siku ngumi zinachapwa mtaa huu na mtaa ule. Unazibuliwa ngumi ya shingo, akisemelea nyumbani anabalaswa na bakora. 

Kwanini analialia kibwege badala ya kupigana na wewe? Sihamasishi ugomvi bali nahamasisha hulka za kiume kwa watoto wa kiume. Ndo maana dunia ya sasa wanawake wanashinda kila kitu na watoto wa kiume wanashindwa kila kitu. Tuna kazi kama washua kuweka sawa hili kwa sababu tumeharibu pakubwa sana.

Tunapomjenga mtoto wa kike tusimuue mtoto wa kiume. Kama wazazi wetu walikuwa watu wema na wenye hekima kwa malezi yale. Kwanini leo yake malezi yawe ni ushamba na kupitwa na wakati? Kama kuishi vile tulipata viongozi bora, kwanini tuishi kama nyanya za Ilula? Laini laini?