Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Bendera ya ligi yetu ilivyopepea Morocco

Makala ya 35 ya mashindano ya soka kutafuta taifa bingwa barani Afrika, AFCON 2025, yanaendelea huko Morocco katika viwanja nane tofauti.

Jumla ya maataifa 24 yameshiriki huku kila moja likitakiwa kuwa na wachezaji 28. Hii ina maana kwamba jumla ya wachezaji 672 wameshiriki. Wachezaji hawa ni kutoka ligi mbalimbali duniani, za madaraja tofauti. Mpangilio wa idadi ya wachezaji na ligi zao ni kama ifuatavyo

- Ufaransa: 79 (11.9%)

- England: 50 (7.53%)

- Afrika Kusini: 32 (4.82%)

- Misri: 31 (4.67%)

- Hispania: 29 (4.37%)

- Uturuki: 28 (4.22%)

- Italia: 26 (3.92%)

- Tanzania: 25 (3.77%)

- Ujerumani: 21 (3.16%)

- Botswana: 21 (3.16%)


Ligi ya Tanzania inashika nafasi ya tatu kwa ligi za Afrika zilizotoa wachezaji wengi kwenye AFCON hii, nyuma ya Misri na Afrika Kusini tu. Hili ni jambo la kujipongeza sana kwa sababu inaonesha kwamba ligi yetu ni bora na imara.

Ukiacha wachezaji wa timu ya taifa ya Tanzania, kuna wengine kadhaa kutoka mataifa mengine wapo huko.

Djigui Diarra - Yanga (Mali)

Khalid Aucho - Singida Black Stars (Uganda)

Prince Dube - Yanga (Zimbabwe)

Steven Mukwala - Simba (Uganda)

Zaidi ya wachezaji, kuna watu wengine kama Riedoh Berdien wa Simba ambaye ni kocha wa viungo wa Burkina Faso. Pia kuna wale ambao kwa sasa hawapo Tanzania, lakini waliwahi kuwa hapa nchini.


Wachezaji

Fiston Mayele (DRC) - alikuwa Yanga 2021 - 2023.

Che Malone (Cameroon) alikuwa Simba 2023 - 2025.

Aziz Ki (Burkina Faso) alikuwa Yanga 2022 - 2025.

Kennedy Musonda (Zambia) - alikuwa Simba 2023 - 2025.


Makocha

Mario Marinika - kocha mkuu Zimbabwe, alikuwa Azam kocha msaidizi wa Azam FC msimu wa 2015/16.

Thom Saintfiet - kocha mkuu Mali, alikuwa Yanga mwaka 2012.

Chlouha Zakaria - Kocha wa makipa wa Morocco, alikuwa kocha wa makipa wa Simba 2024/25.


AFCON 1980 LAGOS NIGERIA

Tanzania ilifuzu kwa mara ya kwanza kushiriki AFCON ya 1980 iliyofanyika Lagos Nigeria.

Hapa ndio ilikuwa mara ya kwanza lifi ya Tanzania kuwakilishwa.

Kikosi chote cha Stars kilijaa wachezaji kutoka ligi yetu.

Athuman Mambosasa - Nyota Morogoro

Leopold 'Tasso' Mukebezi - Balimi FC Kagera

Mohamed 'Machela' Kajole - Simba SC

Leodeger Tenga - Pan Africa

Jellah Mtagwa - Pan Africa

Juma Mkambi - Nyota Mtwara

Omary Hussein 'Keagan' - Yanga

Hussein Ngurungu - Nyota Nyekundu

Peter Tino - African Sports Tanga

Mohamed 'Adolf' Rishard - Pan Africa

Thuwen Waziri Ally - Simba SC

Juma Pondamali - Pan Africa

Idd Pazi - Majimaji Songea

Daud Salum 'Bruce Lee' - Simba SC

Ahmad Amasha - Tumbaku Morogoro

Salim Amir - Coastal Union

Rashid Idd Chama - Yanga

Mtemi Ramadhan - Majimaji

Willy Kiango - Coastal Union

Mohamed Salim - Coastal Union


AFCON 2017 GABON

Baada ya 1980, ligi ya Tanzania haikuwakilishwa tena kwenye AFCON hadi 2017 pale ligi ya Tanzania ilipowakilishwa na wachezaji wawili.

Juuko Murshid wa Simba aliyeshiriki akiwa na taifa lake la Uganda.

Na Bruce Kangwa wa Azam FC aliyeshiriki na taifa lake la Zimbabwe.

Hii ilikuwa AFCON iliyofanyika nchini Gabon. Awali ilipangwa kufanyika Libya lakini vita vya wenyewe kwa wenyewe vikailazimu CAF kuhamisha mashindano.


AFCON 2019 MISRI

Tanzania ilifuzu kwa mara ya kwanza baada ya takribani miaka 40, na kwenda na wachezaji 15 kutoka ligi ya ndani

Aishi Manula - Simba SC.

Metacha Mnata - Mbao FC.

Aron Kalambo - Tz Prisons.

Vicent Philipo - Mbao FC.

Gadiel Michael - Yanga SC.

Ally Mtoni - Lipuli FC.

Mohamed Hussein - Simba SC.

David Mwantika - Azam FC

Kelvin Yondan - Yanga

Erasto Nyoni - Simba SC.

Feisal Salum - Yanga SC.

Mudathir Yahya - Azam FC.

Frank Domayo – Azam FC

John Bocco – Simba SC.

Pia walikuwepo wengine watatu kutoka timu ya taifa ya Uganda, The Cranes.

Emmauel Okwi - Simba SC

Juuko Murshid - Simba SC

Nicholas Wadada - Azam FC

Na pia alikuwepo Thaban Kamusoko wa Yanga akiiwakilisha Zimbabwe.


AFCON 2021 CAMEROON

Safari hii ligi ya Tanzania iliwakilishwa na wachezaji watatu wa Zimbabwe kutoka Azam FC.

Bruce Kangwa

Prince Dube

Never Tigere


AFCON 2023

Tanzania ilifuzu tena safari hii na kuchukua wachezaji 11 kutoka ligi ya nyumbani.

Mudathir Yahya - Yanga

Ibrahim Hamad - Yanga

Dickson Job - Yanga

Feisal Salum - Azam FC

Bakari Mwamnyeto - Yanga

Beno Kakolanya - Singida Black Stars

Mohamed Hussein - Simba FC

Sospeter Bajana - Azam FC

Lusajo Mwaikenda - Azam FC

Aishi Manula - Simba

Mzamiru Yassin - Simba

Kibu Denis - Simba

Abdulmalik Zakaria- Namungo

Lakini pia kulikuwa na wengine kutoka mataifa tofauti wakicheza Tanzania.

Stephane Aziz Ki wa Yanga alikuwa na Burkina Faso.

Djigui Diarra wa Yanga alikuwa na Mali.

Henock Inonga wa Simba alikuwa na DRC.

Na Zambia ilikuwa na wawili, Clatous Chama wa Simba na Kennedy Musonda wa Yanga.

Baeki wa Taifa Stars, Bakar Nondo akijaribu kumtoka beki a Morocoo, Noussair Mazraoui. Picha na Mtandao

Hitimisho

Ligi ya Tanzania inatajwa kama moja ya ligi bora barani Afrika, mambo kama.haya ndio ushahidi.

Unapokuwa na ligi ambayo wachezaji wake wanategemewa na mataifa yaliyopiga hatua kwa kuzalisha vipaji vikubwa, maana yake una kitu.

Na haya yote yameanza 2017, mwaka ambao Wallace Karia alianza kuwa Rais wa TFF.

Sasa Tanzania inafuzu AFCON bila shida. Klabu zale zinafuzu hatua ya makundi bila shida.

Na wachezaji wanaocheza Tanzania wanazitumikia nchi kubwa bila shida

Hapana shaka kwamba ligi yetu ni ligi bora hasa.