Kamati ya Ustawi na Maendeleo ya Jamii imeshauri Serikali kutoa fedha zote zinazopangwa kwa ajili ya mikopo kwa vijana baada ya kubaini katika kipindi cha miaka mitano ni asilimia 20 tu ya fedha ndizo zimetolewa.
Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Fatma Toufiq ameyasema hayo leo Jumatano Aprili 5, 2023 wakati akiwasilisha maoni kuhusu bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Ajira na Wenye Ulemavu kwa mwaka 2023/2024.
Amesema kamati ilibaini kuwa katika kipindi cha miaka kuanzia mwaka 2015/2016 hadi 2020/2021 Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Ajira na Wenye Ulemavu ilitengewa Sh5 bilionii lakini katika kipindi hicho imepokea Sh1 bilioni sawa na asilimia 20 tu ya fedha zilizotengwa kwa kipindi husika.