Miaka 20 ya Premier Agencies katika kutoa huduma bora na kulipa kodi

Mkurugenzi Mkuu wa Premier Agencies, Robert Singu (kulia) akikabidhiwa cheti cha ushiriki wa tuzo za mlipa kodi bora wa mwaka zilizotolewa na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA). Kampuni hiyo ilishika nafasi ya tatu katika kipengele cha walipa kodi wadogo Mkoa wa kikodi wa Temeke.

Muktasari:

Kodi ni msingi wa maende­leo ya Taifa kwa sababu ndizo zinazotumika katika kuten­geneza ustawi wa Taifa kwa kuboresha huduma za jamii na miundombinu.

Kodi ni msingi wa maende­leo ya Taifa kwa sababu ndizo zinazotumika katika kuten­geneza ustawi wa Taifa kwa kuboresha huduma za jamii na miundombinu.

Kodi hizi hulipwa na watu binafsi kupitia shughuli zao iki­wemo ajira, kampuni, mashiri­ka, taasisi wajasiriamali na wafanyabiashara ambao kwa jina moja wote hutambulika kama walipa kodi.

Walipa kodi ni kundi muhimu katika ukuaji wa uchumi na maendeleo kwa sababu kodi ndizo zinaiweze­sha Serikali kutekeleza mam­bo mbalimbali ya kimaende­leo.

Kwa kutambua umuhimu wa walipa kodi Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) ilitan­gaza Novemba kuwa mwezi maalumu kwa ajili ya kutoa shukrani kwao.

Pamoja na mambo mengine mamlaka hiyo ililenga kurudi­sha shukrani kwa walipa kodi na wadau wa kodi wote nchini kwa juhudi na mchango wao katika maendeleo ya Taifa.

Miongoni mwa mambo ambayo TRA wameyafanya ikiwa ni sehemu ya sherehe za maadhimisho hayo ni kuandaa mbio na matembezi ya shukrani kwa mlipakodi pamoja na tuzo ambazo wal­izotoa kwa walipa kodi bora katika makundi tofauti.

Moja ya washindi katika tuzo hizo ni kampuni ya Pre­mier Agencies ambayo ilishika nafasi ya tatu katika kundi la walipa kodi wadogo Mkoa wa Kikodi wa Temeke.

Gazeti hili lilipata nafasi ya kufanya mahojiano na Mku­rugenziwa Mkuu wa kampuni hiyo, Robert Singu ambaye alieleza siri ya mafanikio ya kutwaa tuzo hiyo pamoja na mikakati yao katika kuhakiki­sha wanaendelea kufanya vizuri katika ulipaji kodi.

Tueleze kuhusu Premier Agencies na shughuli inazo­fanya

Premier Agencies ni kampuni iliyoanzishwa mwaka 2002 ambayo inajishughulisha na uuzaji, usambazaji, ufungaji na matengenezo ya vifaa vya kampuni za mafuta na viwandani.

Lengo kubwa la kuanzishwa kwake ni kutoa huduma za matengenezo katika kampuni za mafuta. Pia ni wakandarasi wa daraja la kwanza katika sekta ya mafuta na Gesi (Spe­cialized contractors in oil and gas class 1).

Kitu kilichosababisha kuanzisha kampuni hii ni fur­sa tuliyoiona katika sekta ya mafuta na shughuli za viwan­dani kwa sababu kabla sija­fungua kampuni hii nilifanya kazi katika kampuni za mafuta kwa miaka mingi hivyo niliona fursa hii.

Siku za nyuma wakati nipo katika shughuli za mafuta nilikuwa naona kampuni hizo zikiagiza vifaa, kufunga na kufanya matengenezo zenyewe.

Mkurugenzi Mkuu wa Premier Agencies, Robert Singu akiwa na cheti cha ushiriki wa tuzo za mlipa kodi bora wa mwaka zilizotolewa na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA). Kampuni hiyo ilishika nafasi ya tatu katika kipengele cha walipa kodi wadogo Mkoa wa kikodi wa Temeke.

Baadaye kampuni hizo zil­iamua kupeleka kazi hizo katika kampuni nyingine ili zenyewe ziendeleze biashara ya mafuta hapo ndipo nili­poona fursa hiyo kwa sababu kipindi hicho nilikuwa nafanya kazi katika idara ya maten­genezo kwenye moja ya kam­puni hizo.

Nini kinafanya Premier Agencies kuwa bora sokoni?

Premier Agencies in wakala wa mauzo aliyeidhinishwa wa kampumi mbalimbali kubwa za kimataifa (zilipo Marekani na Ulaya) zinozotengeneza vifaa/mashine mbalimbali mfano Dover fuelling solu­tions, pampu za vituo vya mafuta, Technip FMC, mita za mafuta na gesi.

Ukiwa wakala aliyeidhin­ishwa wa kampuni hizi kubwa unapata nafasi ya wafanyaka­zi wako kupewa mafunzo ya kujengewa uwezo wa namna ya kutambua vifaa halisi na visivyo halisi, ufungaji, maten­genezo nk. Hivyo hili limetu­fanya kuwa moja ya kampuni inayotoa huduma za kipekee na kuaminiwa zaidi.

Premier Agencies haiuzi bidhaa pekee bali pia inatoa huduma za ufungaji, maten­genezo na huduma kwa mteja baada ya mauzo hivyo kui­fanya kuwa ya kipekee katika soko.

Bidhaa zetu zina ubora wa aina moja kwa sababu zin­azalishwa na kampuni moja ambayo viwango vya bidhaa zake viko sawa. Kitu kingine ni weledi ambao tunao katika kutoa huduma.

Ubora wa bidhaa na huduma za Premier Agencies ukoje?

Ubora wa bidhaa zetu ni wa hali ya juu kwa sababu zime­thibitishwa na mamlaka zote za ndani pamoja na mashirika ya kimataifa kwa sababu kam­puni ambazo tunafanya nazo kazi ni za hadhi ya kimataifa.

Bidhaa ambayo inauzwa na Premier Agencies Tanzania ukienda Marekani ama Uin­gereza utaikuta tena katika ubora ule ule kwa sababu viwango vya ubora wa bidhaa za kampuni tunazofanya nazo kazi viko sawa dunia nzima.

Tuzo ya TRA mliyoipata ina maana gani kwenu?

Kwanza tunawashukuru wote waliotupigia kura, tunawaambia kwamba tunathamini imani yao kwetu na tunawahakikishia tutail­inda kwa kuendelea kuwapa huduma bora.

Aidha, TRA kututambua kwamba tunafuata taratibu za kodi imetupa moyo na hamasa ya kuendelea kufuata sheria za kodi nchini kwa sababu sisi tunafanya kazi na kampuni za kimataifa ambazo zinazinga­tia kufuata taratibu, sheria na kanuni zote ikiwemo za kodi ili ziweze kufanya biashara na wewe.

Hivyo tuzo hii imetuon­gezea kuaminika kwa washiri­ka wetu lakini pia Serikali na wateja wetu kwa sababu ime­onyesha ni namna gani tunatii sheria zilizowekwa na mamla­ka husika. Tuzo hii na nyingine ambazo tumewahi kushinda ikiwemo zile za kampuni ndo­go na za kati (Top 100) zimeni­fanya kuwa mwanachama wa Umoja wa Watendaji Wakuu Tanzania (CEOrt Tanzania) ambao unasimamia maadili ya utendaji kazi.

Ni uzoefu gani mmeupata kwa kushiriki tuzo hizi?

Kikubwa ni kukutana na mashirika na taasisi kubwa zinazofanya biashara nchini, kukaa meza moja na kubadil­ishana uzoefu ni jambo kubwa ambalo tumelipata kwa kush­iriki tuzo hizi.

Mikakati yenu ni ipi katika kuendelea kufanya vizuri kwe­nye tuzo hizi mwakani?

Mkakati mkubwa ni kuen­delea kuboresha mifumo yetu ya ndani hususani ile ya kidiji­tali ili kuhakikisha inaendelea kuwa bora jambo litakalorahi­sisha utekelezaji wa masuala mbalimbali ya kokodi na hivyo kutufanya kuendelea tulip­oishia mwaka huu.

Kingine ni kuendelea kuboresha utoaji wa huduma na bidhaa kwa wateja wetu. Tutahakikisha tulichofanya mwaka huu tunakifanya mara mbili au tatu hapo mwakani hivyo wateja na washirika wetu wakae mkao wa kula mambo mazuri yanakuja.