Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Mzee Mwinyi augua, alazwa hospitalini

Da es Salaam. Rais mstaafu wa awamu ya pili, Ali Hassan Mwinyi amepelekwa hospitali akiugua maradhi ya kifua.

Taarifa kwa umma iliyotolewa na msemaji wa familia, Abdullah Ali Mwinyi imeeleza kuwa, Rais huyo mstaafu, anaendelea kupata matibabu chini ya uangalizi wa karibu wa madaktari.

Kutokana na ushauri wa madaktari wake, familia imeona ni vyema apate faragha akiwa anapatiwa matibabu. Hivyo familia inaiomba jamii kumkumbuka kwenye dua, swala na maombi, imesema taarifa hiyo iliyotolewa usiku huu.

"Kutokana na ushauri wa madaktari wake, familia imeona ni vyema apate faragha akiwa anapatiwa matibabu. Hivyo Familia inaiomba jamii kumkumbuka kwenye Dua, Sala, na Maombi.

"Tunamuomba Mwenyezi Mungu amjaalie shifaa ya haraka Mzee wetu pamoja na wagonjwa wengine wote wanaokabiliwa na maradhi mbali mbali." taarifa hiyo imesema.

Mwinyi aliwahi kuwa Waziri wa Mambo ya ndani katika utawala wa Julius Nyerere kisha akawa Rais wa Zanzibar na Rais wa awamu ya pili wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.


Endelea kufuatilia Mwananchi na mitandao yetu kwa habari zaidi.