Pogba akoleza kiduku chake

Muktasari:

  • Pogba anatumikia adhabui ya kukosa mechi tatu baada ya kumchezea vibaya beki  wa Arsenal, Hector Bellerin.

Mshambuliaji  wa Manchester United, Paul Pobga anayetumiakia adhabu ya kukosa mechi tatu, amegeukia mitindo ya nywele ambapo ameonekana akiwa amekoleza rangi kwenye kiduku chake.

Mchezaji huyo aliikosa mechi ya watani ya Manchester United na Manchester City Jumapili iliyopita na hakuwepo kabisa uwanjani. Pia ameikosa mechi ya United na Bournemouth.

Jana Alhamisi, mchezaji huyo mwenye mika 24 alituma picha yake akionyesha mtindo mpya wa nywele kwenye ukurasa wake wa Instagram.

Hata hivyo, mchezaji huyo amekuwa akijifua mazoezi binafsi ili kuhakikissha anajiweka fiti na mechi zinazofuata.