Ecobank yazindua njia salama ya malipo kwa mtandao

Mkuu wa Kitengo cha wateja wa Reja Reja wa Ecobank Ndabu Lilian akizungumza wakati wa Uzinduzi  huduma ya Malipo kwa njia ya Mtandao, inayayojulikana kama MasterPass na Mvisa. Ecobank Tanzania ni Benki ya kwanza nchini kuzindua huduma ya Mobile App ambayo inakuwa ni suluhisho kwa huduma za kifedha.

Muktasari:

  • Yaanzisha mfumo mpya ambao utawanufaisha wateja na wasio wateja kufanya malipo kwa urahisi kwenye maduka

Dar es Salaam. Ecobank imeboresha aplikesheni yake ya simu za mkoni kwa kuanzisha utaratibu utakaowawezesha watu kulipia bidhaa moja kwa moja kupitia simku zao za mkoni.

Akizungumza jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi Mtendaji wa Ecobank Tanzania, Mwanahiba Mzee, amesema hatua hiyo inalenga kuwarahisisha wateja wa benki na watu wengine kudhibiti fedha zao.

Applikesheni hiyo ya simu za mkononi inayojulikana kama Ecobank Mobile App, imekuja na huduma mpya za  MASTERPASS na MVISA ambazo zinamwezehsa mmilikiw a simu ya mkononi kulipia bidhaa na huduma kupitia simu yake.

“Mtanzania yeyote ataweza kutumia teknolojia hii ya mpya kulipia gharama mbali mbali kwa kutumia simu ya mkononi kwa kutumia kodi iitwayo Quick Response au QR,” amesema.

Applikesheni ya Ecobank Mobile ilizinduliwa Februari mwaka huu lakini kwa sasa imeboreshwa zaidi ili wateja wa Ecobank na wasio wateja wa bank waweze kuitumia duniani kote.

“Applikesheni ya Ecobank Mobile App ni njia rahisi ya kujipatia huduma za kibenki ndani ya nchi 33 ambazo Benki yetu inafanya biashara lakini pia unaweza kuitumia ukiwa kokote duniani,” ameongeza.

Kwa upande wake, mkuu wa kitengo cha wateja binafsi, Swere Ndabu, amesema: “Ili kutumia huduma hii wateja wa Ecobank na wasio wateja wanatakiwa kupakua Applikesheni ya Ecobank Mobile App kwenye smartphone zao kisha wanajisajili kwa kutumia kadi ya Visa au Master au kufungua akaunti ya Ecobank Xpress papo hapo na kuanza kufanya miamala ya malipo.”

Swere aliongeza kuwa kwa kutumia Ecobank Mobile App, mteja anaweza kuhamisha fedha kwenye akaunti yake ya Ecobank akiwa hapa nchini au nje ya nchi, pia ataweza kuhamisha fedha kwenda benki nyingine ndsni ay nje ya nchi au kwenda kwenye kadi za Visa duniani kote.

“Pia huduma hii itamwezesha kuunganishwa na huduma za kifedha za simu za mkononi za M-Pesa, Tigo Pesa na Airtel Money,” amesema.