Bunge Kenya lapitisha mkataba wa Epa

Muktasari:

Gazeti la Daily Nation limeripoti kuwa makubaliano hayo yamepitishwa na Bunge.

Dar es Salaam. Wakati nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki zikiwa zimejipa muda kutafakari Makubaliano ya Ushirikiano wa Kiuchumi na Jumuiya ya Ulaya, Bunge la Kenya limepitisha uamuzi wa kusaini mkataba huo.

Katika kikao cha dharura kilichofanyika jijini Dar es Salaam Septemba 9, wakuu wa nchi zinazounda EAC waliamua kujipa muda wa miezi mitatu kutafakari kwa kina makubaliano hayo, yanayoitwa EAC-EU Economic Partnership Agreements(Epa), kabla ya kufanya uamuzi wa mwisho.

Gazeti la Daily Nation limeripoti kuwa makubaliano hayo yamepitishwa na Bunge.

Kenya, inayozisukuma nchi nyingine za jumuiya kusaini makubaliano hayo ambayo, miongoni mwa vipengele vyake yanaruhusu bidhaa kutoka nchi wanachama wa EU kuingia bila ya ushuru, iliitisha kikao cha dharura cha Bunge kwa ajili ya kujadili suala hilo jana.