Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Madiwani wawili Chadema washikiliwa polisi

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Songwe, Mathias Nyange.

Muktasari:

  • Madiwani hao wawili wanatuhumiwa kwa makosa ya jinai.

Madiwani wawili wa Chadema Emmanuel Mwalupasa na Jailo Mwandute katika Halmashauri ya Mji wa Tunduma wilayani Momba wanashikiliwa na polisi  wakituhumiwa kwa makosa tofauti ya jinai.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Songwe, Mathias Nyange amesema Mwalupasa ambaye ni diwani wa Mpande anatuhumiwa kufunga ofisi ya mtendaji kata kwa siku tatu mfululizo.

Kuhusu diwani Mwandute wa Kata ya Katete, amesema anatuhumiwa kwa wizi wa zaidi ya Sh10 milioni ambazo ni kwa ajili ya maendeleo ya kata hiyo. 

Kamanda Nyange amesema madiwani hao  walikamatwa jana Alhamisi jioni na kufikishwa kituo kikuu cha polisi mjini Tunduma ambako wanaendelea kushikiliwa.

Amesema wanaendelea na uchunguzi kuhusu tuhuma zinazowakabili madiwani hao.