NEC yazifutia matokeo wilaya nne

Muktasari:

  • Wilaya hizo zitaanza upya mchakato wa uchaguzi huo 

Dar es Salaam. Mkutano Mkuu wa Halmashauri  Kuu ya Chama cha Mapinduzi Taifa (NEC), umefuta uchaguzi wa wenyeviti katika wilaya nne baada ya kubaini wagombea waliojitokeza hawakua na sifa.

Akitangaza uamuzi huo leo , Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Humphrey Polepole, amezitaja wilaya hizo zilizofutiwa uchaguzi kwamba ni Moshi Mjini,  Siha, Hai,  pamoja na Makete.

Amesema sababu ya kufuta matokeo hayo ni kubainika kwamba  wagombea waliojitokea hawakuwa na  sifa, pamoja na kubainika kuwepo na viashiria hatarishi kwa chama.