Watumishi wawili TRA washikiliwa kuhusika na dawa za kulevya

Muktasari:

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, kamishna wa operesheni wa mamlaka hiyo, Mihayo Msikela alisema watumishi hao walishirikiana na wanaosafirisha dawa hizo kuzipitisha hapa nchini.

Dar es Salaam. Mamlaka ya Udhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya inawashikilia watumishi wawili wa Mamlaka ya Mapato Tanzania(TRA) kwa kuhusika kupitisha viuatilifu vya kutengeneza dawa za kulevya.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, kamishna wa operesheni wa mamlaka hiyo, Mihayo Msikela alisema watumishi hao walishirikiana na wanaosafirisha dawa hizo kuzipitisha hapa nchini.

Alisema watumishi wengine wawili wanafuatiliwa nyendo zao kabla ya kutiwa nguvuni kwa ajili ya mahojiano.