Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

VIDEO: Kaka azuia ndoa ya Samatta isitangazwe

Muktasari:

  • Baba mzazi wa Mbwana Samatta ametolea ufafanuzi wa kwanini alishindwa kuweka wazi jambo la mwanae kuoa kwa majirani zake, akiwataka kutambua staa huyo atabakia kuwa mtoto wao waliomlea kwa namna moja ama nyingine.

BABA  mzazi wa Mbwana Samatta,amefafanua hali halisi iliofanya ashindwe kujumuika na majirani zake kwenye ndoa ya mwanaye iliofungwa jana Alhamisi usiku, Mtongani eneo la Kichangani, Dar es Salaam.
Samatta anayekipiga Genk ya Ubeligiji, amemuoa mchumba wake wa muda mrefu Naima Mgange ambaye amezaa naye watoto wawili.
Ndoa hiyo ilikuwa ya kimyakimya, baada ya Mwanaspoti kufichua hilo, majirani wamemlalamikia mzee Ally Pazi Samatta kwamba hajawatendea haki.
Mzee huyo amejitetea kuwa wakati kaka yake Mbwana, Mohamed Samatta anayecheza KMC anafunga ndoa, kulikuwa na vurugu kubwa ambazo zilifanya maharusi wasahaurike.
"Samatta alihudhuria ndoa ya kaka yake, majirani wote walikuwa wanamshangilia Mbwana na sio Mohamed, sasa nikafikiria hili litakuaje,"
"Sikua na nia mbaya, Mbwana ni mtoto wao ndio maana huwa anakuja kuwatembelea na kuwasalimia, nilitaka wajue nilihofia fujo,"
"Mfano Wanahabari wangetangaza unadhani ingekuaje hapa, pamoja na kimyakimya umeona jinsi nyomi ya watu ilivyokuwa imejaa kwa mwanamke,"anasema.