Davido: Mafanikio yangu ndio sababu ya kuchukiwa
Muktasari:
Mwanamuziki wa Nigeria, Davido amedai wasanii wenzake wana chuki naye kwa kuwa amekuwa na mafanikio makubwa katika muziki
Nigeria. Mwanamuziki wa Nigeria, Davido amedai wasanii wenzake wana chuki naye kwa kuwa amekuwa na mafanikio makubwa katika muziki.
Kupitia ukurasa wa mtandao wake wa kijamii wa Instagram, Davido ameweka video fupi na kuandika kuwa anapenda kuwashukuru mashabiki wanaomuunga mkono na kumpenda baada ya kuachia wimbo aliomshirikisha msanii wa Marekani, Chris Brown.
Davido ameeleza kuwa yupo tayari kuzungumza kuhusu soko la muziki nchini Nigeria kwa kuwa analijua kwa zaidi ya miaka saba lakini hawajamuunga mkono kwa sababu ya chuki.
Kauli hiyo ya Davido imeonekana ni kama kijembe kwa wasanii wenzake nchini Nigeria.
“Wasanii wananichukia kwa sababu nilipewa fedha nyingi na baba kwa ajili ya kufanya muziki, kufanya vizuri na kutoa kazi nzuri. Pamoja na kuwateka mashabiki na hilo ndio kosa langu la kuchukiwa,” amesema Davido.