Afya ya Mbowe yaimarika, kuruhusiwa wakati wowote
Muktasari:
Mbowe aliugua ghafla jana alfajiri na kuwahishwa hospitali ya Muhimbili
Dar es Salaam. Afya ya Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe imeimarika na anaweza kuruhusiwa kutoka Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) wakati wowote kuanzia sasa.
Ofisa Uhusiano wa MNH, Neema Mwangomo ameiambia Mcl Digital leo Juni 19, kuwa kiongozi huyo anaendelea vizuri.
"Nimeongea na muuguzi anayemuangalia amesema afya yake iko vizuri na matibabu yake yamekwenda vizuri anaweza kuruhusiwa muda wowote,"amesema Mwangomo.
Hata hivyo, Mbowe ambaye pia ni Mbunge wa Hai, amekataa kuzungumza na wanahabari.
Soma Zaidi: Uchovu ulivyomlaza Mbowe Muhimbili
"Nimeongea naye amenijulisha kuwa hayuko tayari kuzungumza na waandishi wa habari kwa sasa labda baadaye."