Simu milioni 900 hatarini kudukuliwa
Muktasari:
- Watafiti wa ubora wa programu za simu kutoka Kampuni ya Checkpoint, wamebaini upungufu huo baada ya kujaribu kutatua hitilafu iliyowezesha kirusi kuambukiza mamilioni ya simu zilizokuwa na programu zilizoundwa na Kampuni ya Marekani ya Qualcomm.
Dar es Salaam. Watumiaji milioni 900 wa simu zinazotumia mfumo wa Android duniani kote, wapo hatarini kudukuliwa taarifa kwenye simu zao baada ya kubainika nywila (neno la siri) za simu hizo ni fupi na zinawapa wadukuzi fursa ya kuzidhibiti.
Watafiti wa ubora wa programu za simu kutoka Kampuni ya Checkpoint, wamebaini upungufu huo baada ya kujaribu kutatua hitilafu iliyowezesha kirusi kuambukiza mamilioni ya simu zilizokuwa na programu zilizoundwa na Kampuni ya Marekani ya Qualcomm.
Simu za kisasa zinazotumia programu ya Android ambayo hutengenezwa na Kampuni ya Google, ni miongoni mwa zinazotumika zaidi nchini.