Sugu: Samia amenifanya nisitishe kuhamishia biashara Malawi, Afrika Kusini

Sugu: Samia amenifanya nisitishe kuhamishia biashara Malawi, Afrika Kusini

Muktasari:

  • Aliyekuwa mbunge wa Mbeya Mjini (Chadema), Joseph Mbilinyi maarufu Sugu amesitisha mpango wake wa kuhamishia biashara zake mjini Blantyre, Malawi na Afrika Kusini.

Aliyekuwa mbunge wa Mbeya Mjini (Chadema), Joseph Mbilinyi maarufu Sugu amesitisha mpango wake wa kuhamishia biashara zake mjini Blantyre, Malawi na Afrika Kusini.

Kupitia akaunti yake ya mtandao wa kijamii wa Instagram leo Ijumaa Aprili 16, 2021, Sugu amesema amechukua uamuzi huo kuunga mkono hatua zinazochukuliwa na Rais Samia Suluhu Hassan kuweka mazingira wezeshi ya kufanya biashara Tanzania.