Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Benki ya Efatha yafungwa baada ya taarifa ya BoT

Muktasari:

BoT imezifungia benki tano keanzia leo ikiwemo ya Efatha

Dar es Salaam. Benki ya Efatha imefungwa na hakuna mtu anayeruhusiwa kuingia ndani.

Nje ya benki hiyo zimebandikwa barua za Benki Kuu ya Tanzania(BoT) ambazo zinafafanua hatua iliyochukua na kutoa maelekezo kwa watu wenye amana katika benki hiyo.

Kila mteja anayefika anaelekezwa kwenye tangazo lililobandikwa ili kusoma na kupata maelezo zaidi.

Hakuna watu waliofika kupata huduma na benki hiyo inalindwa na kampuni moja ya ulinzi pamoja na askari polisi.