Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Bodi ya mikopo yatoa orodha mpya ya wanafunzi 7,901

Muktasari:

  • Bodi ya Mikopo imetoa orodha ya awamu ya tatu ya wanafunzi 7,901 wa mwaka wa kwanza watakaopata mikopo.

Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HELSB) imetoa orodha ya awamu ya tatu ya wanafunzi 7,901 wa mwaka wa kwanza watakaopata mikopo.

Taarifa iliyowekwa kwenye tovuti ya bodi na kuthibitishwa na Meneja Mawasiliano wa HELSB, Omega Ngole imesema hadi sasa wanafunzi wa mwaka wa kwanza waliopata mikopo ni 29,578. Bodi ilisema jumla ya wanafunzi 30,000 watapata mikopo hiyo.

Katika awamu ya kwanza wanafunzi 10,196 wa mwaka wa kwanza walipata mikopo na awamu ya pili wanafunzi 11,481 walipata.

Ngole akizungumza na Mwananchi leo Jumapili Novemba 5,2017 amesema orodha ya wanafunzi waliopata mikopo inapatikana www.heslb.go.tz.

Amesema bado bodi inaendelea kuchambua majina ya wanafunzi wengine walioomba na taarifa zitatolewa baadaye.