Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

CWT inajivunia kujitoa kwa walimu kunusuru elimu katika janga la Uviko-19

Muktasari:

  • Oktoba 5 kila mwaka ni siku ya mwalimu ambayo huadhimishwa kote duniani kwa ajili ya kuwapongeza walimu kwa kazi kubwa wanayoifan­ya.

Oktoba 5 kila mwaka ni siku ya mwalimu ambayo huadhimishwa kote duniani kwa ajili ya kuwapongeza walimu kwa kazi kubwa wanayoifan­ya.

Hii ni kumbukumbu ya kupitishwa kwa pendekezo la ILO / UNESCO la 1966 kuhu­su hadhi ya walimu, ambayo inaweka vigezo kuhusu haki na majukumu ya walimu, na viwango vya maandalizi yao ya awali, ajira, na mazingira ya kufundishia na kujifunzia.

Siku ya Walimu Duniani imekuwa ikiadhimishwa tan­gu 1994 kwa ushirikiano kati ya Shirika la Kazi Duniani (ILO), UNICEF na Shirikisho la Vyama vya Walimu Duniani (Education International - EI).

Kaulimbiu ya siku ya walimu duniani mwaka huu 2021 ni “Walimu kiini cha kuhuisha elimu”. Kauli mbiu hii imekuja kufuatia kuwepo kwa janga la UVIKO 19 na jinsi walimu walivyopambana kuinusuru elimu katika nchi mbalimbali.

Kipindi cha mwaka mmoja na nusu kilichopita tume­shuhudia dunia ikipita katika janga la Uviko-19 na kuathiri taaluma ya ualimu na utoaji elimu kwa ujumla, hivyo basi siku ya walimu duniani ya 2021 imezingatia zaidi msaa­da mkubwa ambao walimu wameuotoa kikamilifu katika kuhuisha elimu katikati ya janga hili kubwa.

Chama cha walimu Tan­zania kama walivyo wana­chama wengine wa shirikisho a vyama vya walimu duniani kinaungana na walimu wote duniani katika kuadhimisha siku hii muhimu kwa walimu.

Tangu kuanzishwa kwake tarehe Novemba 1, 1993, Chama cha Walimu Tanza­nia kimekuwa kikitekeleza madhumuni yake ambayo ni; Kujenga nguvu ya pamoja katika kudai haki, maslahi na mazingira bora ya kazi, Kuwalinda wafanyakazi kati­ka sehemu zao za kazi dhidi ya uonevu na ukandamiz­aji wa mwajiri, kusuluhisha migogoro ihusuyo ajira zao, kuwawezesha wafanyakazi kutoa maoni yao kuhusu chan­gamoto zinazowakabili katika mazingira yao ya kazi, Kutoa maoni ya jinsi ya kuongeza tija na namna ya kukabiliana na vikwazo katika uzalisha­ji, Kujadili na kupendekeza miundo mizuri ya utumishi.

Chama cha Walimu Tan­zania kimekuwa kikitekeleza majukumu yake ya kumuhu­dumia mwanachama kwa kuz­ingatia katiba, kanuni, sera na miongozo mbalimbali iliyoji­wekea. Shughuli mbalimbali zinazofanywa na CWT zina­jikita katika kuitangaza kauli mbiu yake ambayo ni wajibu na haki.

Mahusiano ya CWT na wana­chama wake

Kwa kipindi cha uwepo wa chama takriban miaka 28 tan­gu kuanzishwa kwake CWT imefanikiwa kufanya baadhi ya mambo yafuatayo:-

Uanzishwaji wa benki ya Mwalimu (MCBL) Julai 2016 inayoendelea kukua na kufikia hatua ya kuanza kupata faida kwa kipindi cha mwaka 2021.

Ili kutekeleza lengo la kuwainua walimu kitaal­amu na kitaaluma CWT Kwa kushirikiana na shirika la Helvetas tunaendesha mra­di wa kuboresha mbinu za kufundishia katika mikoa ya Arusha, Kilimanjaro, Man­yara, Dodoma, Shinyanga, Singida na Tabora.

Kuimarisha mazingira bora ya utendaji kazi kwa kujenga ofisi za Wilaya 38 na ukara­bati wa ofisi 9 kwa “forced account”.

Chama kuwepo, kuendelea kukua na kuimarika kwa kip­indi cha miaka 28 na kuende­lea kuongeza idadi ya wana­chama takribani wanachama laki tatu tangu kuanzishwa kwake.

CWT kwa namna nyingine imeendelea kusaidia wana­chama kutoa elimu kwa njia ya vyombo vya habari kipindi cha janga la Uviko 19 kati ya mwezi Aprili hadi Juni 2020.

Chama kimekuwa kikiende­lea kutoa huduma ya utetezi ikiwa ni pamoja na kutetea walimu kwenye kesi mbalim­bali zinazowakabili walimu mahakamani, ambapo kwa kiwango kikubwa kesi zina­pungua baada ya kuelimishwa na kukumbushwa wajibu wao kama wanachama kwa mwa­jiri/Serikali na jamii.

Wanachama kuendelea kuk­ijua chama chao na kupele­kea kukua kwa demokrasia ambapo kwa mwaka 2020, takwimu zinaonesha walimu waliojitokeza kugombea nafa­si mbalimbali walikuwa Zaidi ya 91,000 sawa na asilimia 45.

Mahusiano ya CWT na Serikali

CWT imefanikiwa kuon­doa ukomo wa madaraja kwa walimu ambapo awali madaraja yetu na vyeo vya walimu yalikuwa na ukomo, kwa mfano mwalimu mwenye cheti ukomo wake kwa kipindi hicho ulikuwa “E”, mwenye stashahada ulikuwa “F”, uko­mo huu uliondolewa na CWT sasa hivi hakuna ukomo.

Majadiliano yaliyofanyika kati ya CWT na Serikali uli­leta vianzia vya mishahara ya wakufunzi wa vyuo vya Ual­imu (Vyuo vya Kati).

Posho za madaraka kwa wakuu wa Vyuo vya kati, maafisa elimu kata, wakuu wa shule na walimu wakuu.

Kufikia Juni 2021 walimu wapatao 121,074 walipanda vyeo kwa bajeti yam waka 2020/2021 na waliobadilishi­wa mshahara hadi tarehe 30 Juni 2021 ni walimu 93,355.

Hitimisho

Kupitia siku ya walimu duniani tunapenda kutoa wito kwa wadau wengine wa eimu nchini kutumia siku hii kwa kufanya tathimini juu ya huduma mbalimbali wanazozitoa kwa walimu na kuangalia njia bora zaidi za kutatua changamoto zinaz­owakabili walimu ili kurahi­sisha kazi yao ya utoaji elimu nchini.

Aidha watumie siku hii pia kutambua kazi za walimu na kuwapa heshima kwa kutam­bua mchango wa mwalimu katika Jamii.

Tunapenda kuwapongeza walimu wote kwa kazi nzuri walizoendelea kuzifanya hasa katika kipindi kigumu cha jan­ga la UVIKO 19.

Tunatoa wito kwao kuen­delea kufanya kazi zao kwa umahiri na kuendelea kulinda afya zao kwa kushiriki kupata chanjo ya Uviko 19 kwa hiari ili kuendelea kulinda nguvu kazi ka