Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Epukeni vishoka: Tanesco yaonya

Muktasari:

Akizungumza  na waandishi wa Habari leo, Mhandisi wa Tanesco,  Majige Mabulla amesema tangu Januari mwaka huu, hadi sasa kumeripotiwa majanga 18 ya moto, yaliyosababishwa na ‘vishoka’ kuunganisha umeme majumbani.

Dar es Salaam. Shirika la Umeme nchini(Tanesco) limesema majanga ya moto yanayotokea majumbani yansababishwa na  uzembe wa wateja na Tanesco wasihukumiwe.

Akizungumza  na waandishi wa Habari leo, Mhandisi wa Tanesco,  Majige Mabulla amesema tangu Januari mwaka huu, hadi sasa kumeripotiwa majanga 18 ya moto, yaliyosababishwa na ‘vishoka’ kuunganisha umeme majumbani.

Amesema matukio ya moto ni adimu kutokea endapo mfumo wa usukaji nyaya katika jengo unafanywa  na wataalamu wenye  ujuzi.

“Matumizi ya vitu kama pasi na mashine za kufulia  na kuchemsha maji ndio chanzo cha moto majumbani hapo tatizo sio la shirika ni la wa tumiaji”amesema.

Amesema Tanesco hutoa fidia kwa wahanga wa majanga yaliyosababishwa na kuongezeka kwa umeme kuliko uwezo wa miundo mbinu ambapo kwa kawaida  tatizo hilo huathiri nyumba zaidi ya moja zilizo katika mkondo huo .

 “Tatizo la umeme kuzidi na kusababisha  hitilafu haliunguzi nyumba moja bali mkondo wote uliounganishwa kwenye mfumo huo,” amesema