Gwajima atinga Clouds na Hammer yake

VIDEO: Gwajima aenda Clouds kuwapa pole

Muktasari:

Kiongozi huyo wa amefika katika ofisi hizo saa 4:00 asubuhi akiwa na msafara wa magari zaidi ya manne naye alikua katika gari aina ya Hammer.

Dar es Salaam. Askofu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat  Gwajima tayari amewasili katika ofisi za Clouds Media GRoup kwa ajili ya kutoa pole kama alivyoahidi.

Kiongozi huyo wa amefika katika ofisi hizo saa 4:00 asubuhi akiwa na msafara wa magari zaidi ya manne naye alikua katika gari aina ya Hammer.

Amepokelewa na mkurugenzi wa vipindi na uzalishaji wa clouds Ruge Mutahaba na sasa yupo katika mazungumzo ya viongozi wa kituo hicho.