Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Historia niijuayo ya Shilingi ya Tanzania

Muktasari:

  • Naweza kusema kuwa nimejua sarafu rasmi ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania tangu ilipoanza kutumika Juni 1966 ikijulikana kama Shilingi. Ni neno kutoka lugha ya Kiingereza.

Naweza kusema kuwa nimejua sarafu rasmi ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania tangu ilipoanza kutumika Juni 1966 ikijulikana kama Shilingi. Ni neno kutoka lugha ya Kiingereza.

Kabla ya hapo, iliyokuwa Tanganyika, pamoja na nchi jirani za Kenya, Uganda, pamoja na Aden na Somaliland zilikuwa zikitumia Shilingi ya Afrika Mashariki, chini ya ya Bodi ya Sarafu ya Afrika Mashariki (EACB East African Currency Board).

Labda ni muhimu kuzingatia kwamba Zanzibar ilijiunga tu na Bodi ya Sarafu ya Afrika Mashariki mwaka 1936 na baadaye, ikaingia kwenye ushiriki wa historia ya sarafu hiyo na Tanganyika hadi leo, nikitumaini ushiriki huo utaendelea pia kwa siku zijazo.

Bodi ya Sarafu ya Afrika Mashariki ilianzishwa na Uingereza mwaka 1919 na kupewa mamlaka ya kutoa na kusimamia sarafu katika ile iliyokuwa ikiitwa Afrika Mashariki ya Uingereza: Kenya Colony, Tanganyika Territory, Uganda Protectorate, kuanzia kwa mwaka 1920.

Awali ofisi zake zilikuwa eneo la 4 Millbank, London SW1 kwa Uingereza, huku ofisi kuu ikiwa Nairobi, Kenya, ambapo makao yake makuu yalihamishiwa huko mwaka 1960,

Kawaida sarafu zilichapishwa na kampuni iliyoitwa ‘Thomas de la Rue & Co Ltd’ ya London, na sarafu hiyo ilikuwa na picha ya Wafalme wa Uingereza pamoja na toleo la pili la Malkia Elizabeth (QE-II), ambaye aliingia kwenye kiti cha enzi mwaka 1952. Hata hivyo, picha yake ilianza kuonekana kwa mara ya kwanza kwenye sarafu za EACB mwaka 1953.

Lakini kwa kipindi kifupi kati ya 1920 na 1921, sarafu iliyotumika katika makoloni ya Uingereza na nchi nyingine zilizokuwa chini ya Waingereza ilikuwa Florin, ambayo ilichukua nafasi ya Rupee ya Ujerumani na yenyewe baadaye nafasi yake kuchukuliwa na Shilingi ya Afrika Mashariki .

Katika siku hizo chini ya Ujerumani, sarafu iliyotumiwa ilikuwa Rupia ya India na Heller ya Ujerumani (Hii ilitoholewa na kuwa ‘Hela’ kwa Kiswahili; ‘Heleri’ kwa Kichagga, na kadhalika, yote hayo yakimaanisha ‘pesa!’)

Kimsingi, Rupia ilikuwa sarafu ya India ambayo ilitengenezwa kutokana na madini ya fedha. Hata hivyo, wakati bei ya fedha ilipopanda kutoka shilingi mbili mwaka 1902 hadi karibu shilingi saba mwaka 1919 wakati wa matukio ya Vita Kuu ya Kwanza vya Dunia (1914-1918), nguvu ilibadilika kutoka Rupia kwenda Florin.

Inavyoonekana, Florin ilikuwa na nguvu kuliko Shilingi, kwani ubadilishaji ulikuwa ni Shilingi mbili kwa Florin moja; Florin kumi kwa Pauni moja ya Uingereza. Haijulikani kabisa kwa nini iliondolewa kwenye matumizi, isipokuwa inawezekana ikawa ni kwa sababu ya bei ya fedha.

Lakini, baada ya Tanganyika, Uganda na Kenya kupata uhuru wa kisiasa kutoka kwa utawala wa Uingereza (Desemba 9, 1961; Oktoba 9, 1962 na Desemba 12, 1963, mtawalia), Bodi ya Sarafu ya Afrika Mashariki ilibadilishwa mwaka 1966 majukumu yake yakachukuliwa na Benki Kuu za nchi hizo tatu huru.

Hivyo ndivyo Shilingi ya Tanzania, Kenya na Uganda zilivyoanza, zote zikiwa na thamani ya Sh20 kwa Pauni ya Uingereza, na Sh7.20 kwa Dola moja ya Marekani.

Kabla ya Serikali ya Uingereza kujitokeza baada ya Uingereza na washirika wake kushinda Vita Kuu ya 1914-18 dhidi ya Ujerumani na washirika wake wengine’ - vita ambayo ilipewa jina la ‘Vita ya Kwanza ya Ulimwengu’ (WW-I), Tanzania Bara ya leo ilikuwa pamoja na Rwanda ya leo, Burundi na Pembetatu ya Kionga huko Msumbiji, zote zilijulikana kama ‘Deutsch Ostafrika’, chini ya utawala wa Ujerumani.

Lakini, muda mrefu kabla ya Waafrika Mashariki kuwasiliana na wafanyabiashara wa nje, jamii za jadi za Kiafrika zilikuwa zikibadilishana bidhaa kwa bidhaa kupitia biashara ya kubadilishana, mfumo ulioanzia nyakati za kale katika historia.

Katika siku za masoko ambazo zilikuwa sehemu ya kimila ya maisha ya kitamaduni vitu muhimu zaidi vya kubadilishana wakati wa biashara ni mifugo, chuma, chumvi, silaha, shanga, maganda ya kauri na chakula. (Tazama https://www.trademarkea.com/news/a-history-of-currency-in-east-africa-from-1895/).

Kama ilivyosemwa hapa juu, Bodi ya Sarafu ya Afrika Mashariki ilivunjwa mwaka 1966, na mfumo wake wa sarafu uliondolewa katika biashara Afrika Mashariki na Shilingi ya Tanzania ikichukua nafasi ya Shilingi ya Afrika Mashariki kuanzia Juni 14, 1966.

Majukumu ya bodi na sarafu yake yalichukuliwa na Benki Kuu za Kenya, Tanzania na Uganda, na hivyo kutoa nafasi kwa Shilingi ya Kenya, Tanzania na Uganda.

Pale mwanzoni, sarafu hizo tatu zilikuwa sawa kwa thamani katika viwango vya kubadilisha fedha lakini kadiri nyakati zilivyopita na mambo yalibadilika.

Kwa mfano, Septemba 23, 2021, Dola ya Marekani ilibadilishwa rasmi kwa Shilingi 110.30 za Kenya (KSh); Shilingi 2,312 za Tanzania (TSh), na Shilingi za Uganda 3,530 (USh).

Kwa upande mwingine, Shilingi moja ya Kenya ni ‘sawa’ na Shilingi 20.97 za Kitanzania na Shilingi 31.97 za Uganda.

Hii peke yake inaonyesha kuwa Shilingi ya Kenya ndiyo sarafu yenye nguvu zaidi katika Jumuiya ya Afrika Mashariki ya nchi sita (EAC) ambayo pia inahesabu Rwanda, Burundi na Sudan Kusini kama nchi wanachama.

Lakini, kwa kumalizia hadithi hii, historia ya sasa ya sarafu ya Tanzania jinsi ninavyoijua, Bodi ya Sarafu ya Afrika Mashariki ilifungwa mwaka 1965, na majukumu yake kuchukuliwa na Benki Kuu ya Tanzania (BoT).

BoT ilianzishwa chini ya Sheria ya Benki ya Tanzania ya 1965, na Edwin Mtei alikua Gavana wake wa kwanza mwaka 1966, wadhifa alioshikilia hadi mwaka 1974.

Hata hivyo, Sheria ya Benki ya Tanzania ya mwaka 1995 iliipa Benki Kuu mamlaka juu ya Sera ya Fedha ya nchi kuhakikisha utulivu wa bei katika mazingira ya fedha, kufuatia uchumi huria ulioongozwa na Rais Benjamin Mkapa wa Serikali ya awamu ya tatu (1995-2005).

Sheria ya BoT ya 1995 ilifafanuliwa zaidi na marekebisho ya 2006, na kwa sasa ndiyo sheria inayoongoza ya Benki Kuu.

Kwa kifupi, ‘Sera ya Fedha’ kimsingi ni kuhusu hatua zilizochukuliwa na Benki Kuu na/au Hazina ya Serikali kuimarisha uchumi wa nchi.

Lakini BoT pia imepewa mamlaka chini ya Sheria ya 2006 na haki pekee ya kutoa noti. Kwa hivyo, Benki inawajibika kubuni na kupata noti na sarafu ili kukidhi mahitaji ya sarafu ya nchi.


Mwandishi anapatikana kwa baruapepe: [email protected]