Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Mikoa hii ijiandae kwa mvua usiku huu 

Picha na Mtandao

Muktasari:

  • Leo Jumapili, Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imetoa tahadhari ya mvua kubwa katika maeneo mbalimbali nchini.

Dar es Salaam. Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imetoa angalizo la mvua na ngurumo kuanzia leo Jumapili Aprili 19,2026 usiku katika mikoa mbalimbali nchini.

Mikoa hiyo ni kutoka visiwa vya Unguja na Pemba, Tanga na Dar es Salaam, kaskazini mwa Mkoa wa Morogoro, Kilimanjaro, Arusha na Manyara na Pwani (ikijumuisha Visiwa vya Mafia).

Mikoa mingine ni ya Mtwara na Lindi, kusini mwa Mkoa wa Morogoro, Kigoma, Katavi na Tabora, Kagera, Geita, Mwanza, Shinyanga, Mara na Simiyu, Dodoma na Singida.

Pia mikoa ya Ruvuma, Rukwa, Songwe, Mbeya, Iringa na Njombe 

Kwa kesho Jumatatu, Aprili 20, 2026, imetoa angalizo la uwepo wa mvua kubwa katika mikoa ya Tanga, Kilimanjaro, Arusha na Manyara pamoja na visiwa vya Unguja na Pemba.

Siku ya Jumanne ya Aprili 21, 2026 TMA haikutoa angalizo lolote la hali ya hewa lakini Aprili 22, kutakuwa na mvua kubwa mkoa wa Tanga na visiwa vya Unguja na Pemba.

Pia Aprili 23, 2026 hakutakuwa na tahadhari yeyote juu ya hali ya hewa kulingana na ratiba iliyotolewa na TMA leo Jumapili, Aprili 19, 2026.