Mkurugenzi Gairo akamatwa na polisi tuhuma wizi wa mabati
Muktasari:
- Mkurugenzi wa halmashauri ya Wilaya ya Gairo, Asajile Mwambambale anashikiliwa na polisi mkoani Morogoro kwa tuhuma ya wizi wa mabati 1,100 mali ya halmashauri ya Wilaya ya Kilosa.
Morogoro. Mkurugenzi wa halmashauri ya Wilaya ya Gairo, Asajile Mwambambale anashikiliwa na polisi mkoani Morogoro kwa tuhuma ya wizi wa mabati 1,100 mali ya halmashauri ya Wilaya ya Kilosa.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro, Fotunatus Muslimu amesema hayo leo Jumanne Agosti 24, 2021 katika mkutano wake na waandishi wa habari.
Muslimu amesema kutokana na wizi huo watu wengine saba wanashikiliwa na wanadaiwa kushirikiana mkurugenzi huyo na wanaendelea kuhojiwa.
Awali Mwambambale alikuwa mkurugenzi wa halmamshari ya Kilosa kabla ya kuhamishwa halmashauri ya Gairo.
Wizi wa mabati hayo ulifanyika Juni 17, 2021 eneo ya ujenzi kitongoji cha Mvumi B wilayani Kilosa katika stoo ya halmashauri hiyo ambayo haikuvinjwa ambapo stoo hiyo haikuvunjwa.