Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Moto wateketeza soko la mbao

Picha ya mtandao. Si ya tukio halisi

Muktasari:

Taarifa kutoka katika eneo la tukio zimebainisha kuwa gari la zimamoto la Mji wa Kahama limefika, lakini kutokana na moto kuwa mkubwa wameomba msaada kutoka kwenye mgodi wa dhahabu wa Buzwagi.

Kahama. Soko la mbao lililoko Kata ya Majengo mjini Kahama limeteketea kwa moto pamoja na kuteketeza mali na vifaa mbalimbali.

Tukio hilo liloanza saa 12 jioni linadaiwa kusababishwa na hitilafu ya umeme.

Taarifa kutoka katika eneo la tukio zimebainisha kuwa gari la zimamoto la Mji wa Kahama limefika, lakini kutokana na moto kuwa mkubwa wameomba msaada kutoka kwenye mgodi wa dhahabu wa Buzwagi.

Soko hilo ambalo lipo karibu na stendi ndogo ya magari, limetengwa maalumu kwa ajili ya kuuzia mbao, kuranda na kuchomelea vifaambalimbal ivya chuma.

Hata hivyo, hakuna taarifa za majeruhi wala vifo katika tukio hilo. Jitihada za kuuzima moto huo zinaendelea.