NMB yazindua Huduma ya Wakala kwa Simu za Mkononi
Muktasari:
- Benki ya NMB imezindua huduma maalumu ya kuweka na kutoa pesa kirahisi kupitia wakala watakao tumia simu zao za mkononi tu.
Benki ya NMB imezindua huduma maalumu ya kuweka na kutoa pesa kirahisi kupitia wakala watakao tumia simu zao za mkononi tu.
Huduma hiyo ya NMB Pesa Wakala imezinduliwa jijini Dar es Salaam, ikilenga kusogeza ‘Karibu Zaidi’ huduma za kifedha kwa wananchi, pamoja na kutoa fursa za ajira kwa Watanzania, lengo likiwa kuongeza idadi ya mawakala kutoka 11,000 wa sasa, hadi 100,000 miaka mitano ijayo.
Akizungum za na waandishi wa habari Afisa Mkuu wa Wateja Binafsi na Biashara wa NMB, Filbert Mponzi amevitaja vigezo vya mtu kuomba uwakala wa NMB Pesa Wakala kuwa ni pamoja na Leseni ya Biashara, Kitambulisho cha Taifa (NIDA) na simu ya mkononi ya aina yoyote (smartphone au kitochi).
“Sasa Wakala anaweza kutumia huduma hii kupitia simu yake ya mkononi tu, bila kuhangaika kupata mashine za PoS ambazo zinatumia kadi. Kwa mteja, hakikisha umejiunga na NMB Mkononi kuweza kufurahia huduma hii kiurahisi”.amesema Mponzi
Mponzi amesema Huu ni muendelezo wa utoaji wa suluhishi za kidigitali zilizo rahisi na salama kwa wateja ili kuwafanya kuendelea kufurahia huduma zao popote walipo.